DUA ZOTE KWA SERENGETI BOYS
 Dua
 na sala za Watanzania zielekezwe pia kwa timu ya Taifa ya Mpira wa 
Miguu ya vijana wenye umri wa chini ya miaka 17 ‘Serengeti Boys’, 
iliyoondoka leo saa 12.00 Uwanja wa Ndege ya Mwalimu Julius K. Nyerere, 
Dar es Salaam, Tanzania kwenda Antananarivo, Madagascar kupitia Uwanja 
wa Ndege wa Ndege ya Oliver Tambo jijini Johannesburg, Afrika Kusini.
Serengeti
 Boys inayokwenda kuweka kambi huko Antananarivo, Madagascar inatarajiwa
 kufika huko saa 8.10 mchana. Timu hiyo inajiandaa kucheza na Afrika 
Kusini katika mchezo wa awali kuwania nafasi ya kucheza fainali za Kombe
 la Mataifa ya Afrika utakaofanyika Agosti 6, 2016.
Mchezo
 wa marudiano utafanyika Agosti 21, mwaka huu kwenye Uwanja wa Azam, 
ulioko Chamazi-Mbagala, nje kidogo ya jiji la Dar es Salaam. Serengeti 
ipo kwenye ushindani wa kuwania nafasi ya kufuzu fainali za Kombe la 
Mataifa ya Afrika kwa vijana, zitakazofanyika mwakani huko Madagascar.
Wakati
 mkuu wa msafara akiwa ni Ayoub Shaibu Nyenzi ambaye ni Mwenyekiti wa 
Kamati ya Soka la Vijana, maofisa wengine waliosafiri na timu hiyo ni 
Kocha Mkuu, Bakari Nyundo Shime, Daktari wa timu hiyo, Shecky Francis 
Mngazija na Mtunza Vifaa, Andrew Vanance Andrew pamoja na Juma Kaseja 
Juma ambaye kwa muda amechukua nafasi ya makocha wasaidizi, Sebastian 
Nkoma na Muharam Mohammed ‘Shilton’ wanaohudhuria kozi ya makocha ngazi 
ya juu inayoratibiwa na CAF.
Nyota
 waliosafiri ni pamoja na makipa, Ramadhani Awm Kabwili, Kelvin 
Deogratius Kayego na Samwel Edward Brazio wakati mabeki wako Kibwana 
Ally Shomari, Nickson Clement Kibabage, Israel Patrick Mwenda, Dickson 
Nickson Job, Ally Hussein Msengi, Issa Abdi Makamba na Enrick Vitalis 
Nkosi.
Viungo
 ni Kelvin Nashon Naftal, Ally Hamisi Ng’anzi, Asadi Ali Juma Ali, 
Syprian Benedictor Mtesigwa, Ibrahim Abdallah Ali, Shaban Zuberi Ada 
huku washambuliaji wakiwa ni Mohammed Abdallah Rashid, Yohana Oscar 
Mkomola na Muhsin Malima Makame.
“Najua
 mchezo utakuwa mgumu, lakini nakiamini kikosi change. Kiko imara,” 
amesema Shime, maarufu zaidi kwa jina la Mchawi Mweusi. 
Serengeti
 Boys inakwenda kucheza na Afrika Kusini baada ya kuwatoa Shelisheli kwa
 jumla ya mabao 9-0 katika mechi zake mbili za kimataifa. Mshindi wa 
jumla kati ya Serengeti Boys na Afrika Kusini, atacheza na timu mshindi 
kati ya Namibia na Congo-Brazaville.
Hivi
 karibuni Serengeti Boys ilifanya ziara India ambako walishiriki 
mashindano ya vijana ya Kimataifa yanayotambuliwa na FIFA (AIFF 
International Youth Tournament 2016) kabla ya kurudi na rekodi ya 
kupigiwa mfano si tu katika Tanzania na kwa nchi za Afrika Mashariki. 
Ilishika nafasi ya tutu nyuma ya Korea Kusini na Marekani.
…..……………………………………………………………………………………………..
IMETOLEWA NA SHIRIKISHO LA MPIRA WA MIGUU TANZANIA
 
 
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni