TDL yazindua kampeni ya shinda gari kanda ya ziwa
……………………………………………………………………………………………..
KAMPUNI  ya  Tanzania 
Distilleries Limited (DTL)  inayotengeneza na kusambaza kinywaji cha 
konyagi imezindua kampeni ya nunua, uza shinda gari  na Konyagi kwa 
wasambazaji wa bidhaa hiyo .
  Akizungumza katika uzinduzi 
wa kampeni hiyo jijini Mwanza juzi, Meneja masoko na Udhamini wa TDL, 
George Kavishe, alisema kampeni hiyo itashindanisha magari mawili yenye 
thamani ya Sh milioni 98 na itadumu kwa muda wa miezi mitatu ikilenga 
kuinua uchumi wa wasambazaji na wauzaji wa bidhaa zao.
Alisema kampeni hiyo itatoa 
washindi wawili na kwamba watakaopatikana kwa kuzingatia vigezo husika 
watakabidhiwa magari aina ya Eicher 3 Tonne Truck.
“Mshindi atajishindia gari aina
 ya Eicher 3 Tonne Truck ambazo zitarahisisha usambazaji  wa biashara 
yake,  hivyo kupitia shindano hili tutakuwa tumeboresha usambazaji wa 
biehaa yetu ya Konyagi, wasambazaji  na wauzaji wetu kutoka Kanda nne 
watashiriki na kila gari ina thamani ya Sh milioni 49.
“Pia kupitia shindano hili kwa 
kuwa tunaimani mauzo yataongezeka itatusaidia kuweza kushiriki kutatua 
changamoto mbalimbali za kijamii na kiuchumi kwa wananchi wa hapa 
nchini,”alisema  Kavishe.
Meneja wa Chapa ya Konyagi, 
Martha Bangu, alisema  katika shindano hilo wasambazaji  na wauzaji wa 
bidhaa hiyo wamewekewa viwango ambapo kiwango cha chini ni katoni  400 
na cha juu ni 30, 000 na washiriki wote watakaokidhi vigezo wataingia 
kenye droo kubwa ya kupata mshindi inayotarajia kufanyika Oktoba mwaka 
huu.
Tunaamini kampeni hii itaongeza
 ufanisi kwa wasambazaji wetu nao wataongeza kiwango cha ununuzi wa 
bidhaa zetu , shindano hili ambalo limeanza Julai mwaka huu litaisha 
mwezi Septemba mwaka huu na  litajumuisha wasambazaji wetu wote waliopo 
mikoa ya kanda ya ziwa,  Nyanda za juu kusini , Kaskazini, Pwani na 
Kati,”alisema Bangu
 
 
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni