 Diwani
 Kata ya Kimara Mhe. Pascal Manota akihamasisha wananchi wa Mtaa wa 
Mavurunza Kata ya Kimara kushirikiana na Wataalam wa masuala ya Ardhi 
ili kuruhu upimaji wa maeneo yao walipofanya mkutano wa uhamasishaji juu
 ya Urasimishaji wa Makazi holela.
Diwani
 Kata ya Kimara Mhe. Pascal Manota akihamasisha wananchi wa Mtaa wa 
Mavurunza Kata ya Kimara kushirikiana na Wataalam wa masuala ya Ardhi 
ili kuruhu upimaji wa maeneo yao walipofanya mkutano wa uhamasishaji juu
 ya Urasimishaji wa Makazi holela. 
  Kaimu
 Mkurugenzi Urasimishaji Makazi holela Bi. Bertha Mlonda akielezea faida
 za urasimishaji katika mkutano wa Uhamasishaji kwa wanachi wa Kata ya 
kimara mtaa wa Mavurunza.
Kaimu
 Mkurugenzi Urasimishaji Makazi holela Bi. Bertha Mlonda akielezea faida
 za urasimishaji katika mkutano wa Uhamasishaji kwa wanachi wa Kata ya 
kimara mtaa wa Mavurunza. 
  Badhi
 ya wakazi wa Mtaa wa Mavurunza waliohudhuria mkutano wa Uhamasishaji 
kuhusiana na Urasimishaji Makazi holela, wakiwasikiliza viongozi wa 
Serikali za Mitaa (Hawako pichani) pamoja na wataalam kutoka Sekta ya 
Ardhi walipokuwa wakitoa elimu kwa wakazi hao.
Badhi
 ya wakazi wa Mtaa wa Mavurunza waliohudhuria mkutano wa Uhamasishaji 
kuhusiana na Urasimishaji Makazi holela, wakiwasikiliza viongozi wa 
Serikali za Mitaa (Hawako pichani) pamoja na wataalam kutoka Sekta ya 
Ardhi walipokuwa wakitoa elimu kwa wakazi hao. 
  Hamza
 Khatibu, Mkazi wa Mtaa wa Mavurunza akiuliza swali kwa viongozi wa 
Serikali za Mitaa na wataalam wa Sekta ya Ardhi walipokuwa katika 
mkutano kuhusiana na Urasimishaji Makazi holela.
Hamza
 Khatibu, Mkazi wa Mtaa wa Mavurunza akiuliza swali kwa viongozi wa 
Serikali za Mitaa na wataalam wa Sekta ya Ardhi walipokuwa katika 
mkutano kuhusiana na Urasimishaji Makazi holela. 
  Alama
 inayotenganisha kiwanja kimoja na kingine inayowekwa na wataalam wa 
upimaji kutoka Wizara ya Ardhi, wakishirikia na wataalam kutoka Manispaa
 ya Kinondoni.
Alama
 inayotenganisha kiwanja kimoja na kingine inayowekwa na wataalam wa 
upimaji kutoka Wizara ya Ardhi, wakishirikia na wataalam kutoka Manispaa
 ya Kinondoni. 
  
  
  Wataalam
 kutoka Wizara ya Ardhi na Manispaa ya Kinondoni wakiandaa ramani za 
maeneo ambayo tayari yamefikiwa kwa ajili ya kupimwa na kurasimisha 
makazi holela katika Kata ya Kimara, Mtaa wa Kilungule B.
Wataalam
 kutoka Wizara ya Ardhi na Manispaa ya Kinondoni wakiandaa ramani za 
maeneo ambayo tayari yamefikiwa kwa ajili ya kupimwa na kurasimisha 
makazi holela katika Kata ya Kimara, Mtaa wa Kilungule B. 
……………………………………………………………………………………………..
Na Mwandishi Wetu
SERIKALI
 imeanza kupima viwanja zaidi ya 25,000 kwa wakazi wa kata za Kimara na 
Saranga zilizopo jijini Dar es Salaam ikiwa ni hatua ya kurasimisha 
makazi holela.
Akizungumza
 kwa nyakati tofauti Kaimu mkurugenzi wa Urasimishaji Makazi Holela Bi. 
Bertha Mlonda amesema, Uendelezaji Miji ni kwa mujibu wa Sheria ya 
MipangoMiji na una faida nyingi kwa wanachi. Alisisitiza kwamba, 
Maendeleo ya sehemu yeyote hutokana na miundombinu ya sehemu husika 
pamoja na huduma za kijamii zinazopatika.
Mlonda
 amewaasa wananchi haswa wa Kata za Kimara na Saranga kutoa ushirikiano 
kwa wataalam ambao wameanza kupima maeneo yao ili kuondokana na tatizo 
la Makazi Holela kwa wakazi hao kwani upimaji huo utabadilisha taswira 
na hadhi ya maeneo yao.
Kwa 
sasa Urasimishaji umeanzia katika Kata za Kimara na Saranga, baada ya 
hapo yatafuata maeneo yote yenye sifa za urasimishaji katika jiji la Dar
 es Salaam, na mikoa yote ya Tanzania. Zoezi hili litakuwa likitekelezwa
 kwa awamu kulingana na maeneo yatakavyobainishwa.
 
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni