Jumapili, 31 Julai 2016

SERIKALI KURASIMISHA MAKAZI HOLELA JIJINI DAR ES SALAAM.

O1Diwani Kata ya Kimara Mhe. Pascal Manota akihamasisha wananchi wa Mtaa wa Mavurunza Kata ya Kimara kushirikiana na Wataalam wa masuala ya Ardhi ili kuruhu upimaji wa maeneo yao walipofanya mkutano wa uhamasishaji juu ya Urasimishaji wa Makazi holela.
O2Kaimu Mkurugenzi Urasimishaji Makazi holela Bi. Bertha Mlonda akielezea faida za urasimishaji katika mkutano wa Uhamasishaji kwa wanachi wa Kata ya kimara mtaa wa Mavurunza.
O3Badhi ya wakazi wa Mtaa wa Mavurunza waliohudhuria mkutano wa Uhamasishaji kuhusiana na Urasimishaji Makazi holela, wakiwasikiliza viongozi wa Serikali za Mitaa (Hawako pichani) pamoja na wataalam kutoka Sekta ya Ardhi walipokuwa wakitoa elimu kwa wakazi hao.
O4Hamza Khatibu, Mkazi wa Mtaa wa Mavurunza akiuliza swali kwa viongozi wa Serikali za Mitaa na wataalam wa Sekta ya Ardhi walipokuwa katika mkutano kuhusiana na Urasimishaji Makazi holela.
O5Alama inayotenganisha kiwanja kimoja na kingine inayowekwa na wataalam wa upimaji kutoka Wizara ya Ardhi, wakishirikia na wataalam kutoka Manispaa ya Kinondoni.
O6 O7 O8Wataalam kutoka Wizara ya Ardhi na Manispaa ya Kinondoni wakiandaa ramani za maeneo ambayo tayari yamefikiwa kwa ajili ya kupimwa na kurasimisha makazi holela katika Kata ya Kimara, Mtaa wa Kilungule B.
……………………………………………………………………………………………..
Na Mwandishi Wetu
SERIKALI imeanza kupima viwanja zaidi ya 25,000 kwa wakazi wa kata za Kimara na Saranga zilizopo jijini Dar es Salaam ikiwa ni hatua ya kurasimisha makazi holela.
Akizungumza kwa nyakati tofauti Kaimu mkurugenzi wa Urasimishaji Makazi Holela Bi. Bertha Mlonda amesema, Uendelezaji Miji ni kwa mujibu wa Sheria ya MipangoMiji na una faida nyingi kwa wanachi. Alisisitiza kwamba, Maendeleo ya sehemu yeyote hutokana na miundombinu ya sehemu husika pamoja na huduma za kijamii zinazopatika.
Mlonda amewaasa wananchi haswa wa Kata za Kimara na Saranga kutoa ushirikiano kwa wataalam ambao wameanza kupima maeneo yao ili kuondokana na tatizo la Makazi Holela kwa wakazi hao kwani upimaji huo utabadilisha taswira na hadhi ya maeneo yao.
Kwa sasa Urasimishaji umeanzia katika Kata za Kimara na Saranga, baada ya hapo yatafuata maeneo yote yenye sifa za urasimishaji katika jiji la Dar es Salaam, na mikoa yote ya Tanzania. Zoezi hili litakuwa likitekelezwa kwa awamu kulingana na maeneo yatakavyobainishwa.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni