Serikali yatenga bilioni 1.6 kwa ajili ya uanzishwaji wa mfumo wa kielekroniki wa kusajili wakazi.
(Picha zote na Benjamin Sawe- Maelezo)
…………………………………………………………………………………………………..
Benjamin Sawe -Maelezo Dar es Salaam.
Serikali
 imetenga Jumla ya shilingi bilioni 1.6 kupitia ofisi ya Taifa ya 
Takwimu na wafadhili wametoa shilingi bilioni 1.4 kwa ajili ya 
uanzishwaji wa mfumo wa kielekroniki wa kusajili wakazi Tanzania
Hayo 
yamesemwa na Katibu Mkuu Ofisi ya Rais- TAMISEMI Injinia Mussa Iyombe 
wakati wa kupokea maendeleo ya mfumo wa kuboresha upatikanaji wa taarifa
 sahihi katika serikali za mitaa.
Injinia
 Iyombe alisema mfumo huo unalenga kuwa na kanzi data ya watu wote 
nchini kiumri, uraia, jinsia, hali ya ulemavu, hali ya elimu, shughuli 
za kiuchumi, uhamaji na uhamiaji ikiwa ni pamoja ikiwa na vizazi na 
vifo.
“Taarifa
 hizi zitaisaidia serikali na wadau wengine kujibu maswali ambayo 
wengine tumekuwa tukijiuliza kila siku”.Alsema Injini Iyombe.
Alisema
 katika kutekeleza malengo Endelevu ya Maendeleo ya Mwaka 2030 serikal;I
 haina budi kuhakikisha wananchi wanaandikishwa katika rejesta ya wakazi
 ili iweze kuwafahamu mahitaji yake.
Aliongezea
 kuwa mfumo huo utasaidia upatikanaji wa idadi kamili ya wanafunzi 
waliopo mashuleni na kiasi gani cha fedha kinachotitajika kupelekwa 
shuleni, upatikanaji wa hali halisi ya uandikishaji wa watoto katika 
shule za msingi, mahudhurio shuleni na idadi ya walimu na taarifa 
nyingine.
Alisema
 kwa upande wa TAMISEMI mfumo huo utasaidia kuwagundua wazazi ambao 
hawana nia nzuri ya kuwapeleka watoto kuandikishwa kupitia katika kata 
zao kwa kutumia Global Positioning System za kaya zao katika ramani.
Akielezea
 faida za mfumo huo Injinia Iyombe alisema utaiwezesha serikali kufahamu
 idadi kamili ya watu wake kiumri na kijinsia kwa kuwa kazi hiyo itakuwa
 endelevu na itafanyiwa kazi kila siku na maafisa watendaji wa vijiji na
 mitaa kwa Tanzania nzima kwa kutumia teknolojia ya simu.
Aidha
 mfumo huo utaipa fursa Ofisi ya Takwimu ya kuwa na takwimu bora ambazo 
zitaipunguzia gharama ya kufanya tafiti za kila baada ya miaka mitatu, 
mitano hata kumi ikiwa ni pamoja na kupunguza maswali mengi ambayo 
huulizwa wakati wa sensa wa watu na makazi ambayo itafanyika tena hapa 
nchini mwaka 2022.
 
 
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni