MBUNGE WA JIMBO LA MAGOMENI ZANZIBAR ASHIRIKI UJENZI WA TENKI LA MAJI KATIKA JIMBO LAKE
Picha zote na Makame Mshenga/Maelezo Zanzibar.
…………………………………………………………………………………………….
Na Maryam Kidiko –Husna Sheha / Maelezo Zanzibar.
Mbunge wa Jimbo la Magomeni Jamal 
Kassim Ally amesema changamoto kubwa iliyokuwa inakabili jimbo hilo 
zimeaanza kupata ufumbuzi katika kila shehia ndani ya jimbo .
Ameyasema hayo katika ujenzi wa 
mnara wa maji ndani ya shehia ya sogea jimbo la magomeni wilaya ya mjini
 unguja amesema ujenzi huo ni miongoni mwa ahadi walizozitoa kwa 
wananchi wakati wa kampeni .
Amesema changamoto ya maji 
 ilikuwepo kwa muda mrefu katika shehiya ya sogea jambo ambalo lilikuwa 
likirejesha nyuma maendeleo ya shehia hiyo.
“Tumechukuwa juhudi kubwa na 
viongozi wenzangu kuanzia madiwani na muwakilishi ili kuona suala hili 
linakamilika haraka “ Alisema Jamal.
Aidha amesema wameanzisha mradi wa
 visima vya maji sita katika jimbo hilo ili kuweza kupunguza tatizo la 
ukosefu wa maji  ambalo ni muhimu kwa binaadam kuweza kupata huduma 
hiyo.
Hata hivyo  ametowa fursa kwa 
wananchi wa shehia hiyo kuweka kamati ya visima ili iweze kusimamia 
katika mambo mbali mbali yatayovikabili visima hivyo.
Vile vile amefahamisha kuwa visima
 hivyo vya wananchi wote hivyo kila mwananchi anahaki ya kutumia na 
kuvitunza  visima hivyo bila ya kufanya uharibifu .
Pia amewaomba viongozi 
watakaochaguliwa kusimamia  visima hivyo kuwa na hekma pamoja na busara 
ili kuweza kuepusha migogoro kwa wananchi wataopata huduma hiyo.
Sambamba na hayo amewataka 
wananchi wa jimbo la magomeni mradi huo utapokamilika waweze kutoa 
michango ili kusaidia umeme ambao ndio utaweza kupatikana kwa huduma 
hiyo.
Nae Ramadhan Mwadini mzee ambae ni
 miongoni mwa wa nanchi wa shehia ya sogea jimbo la magomeni amempongeza
 mbunge wa jimbo hilo kwa kuitimiza ahadi aliyoiahidi wakati wa kampeni.
Amewataka viongozi wao wa jimbo kuendelea kutimiza ahadi mbali mbali walizozitoa ili kuweza kuleta maendeleo katika jimbo lao .
Jumla ya visima vinne 
vimeshachibwa kati ya visima sita katika jimbo hilo na kila kisima 
kimegharimu shilingi milioni saba na laki tano.
 
 
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni