JWTZ NETBALL WANAWAKE WAONYESHA UBABE KWA KIKOSI CHA KVZ WANAUME
pichani) katika Kambi ya Bavuai ikiwa ni maandalizi kuelekea Michuano ya Afrika mashariki kwa majeshi
ya nchi za Afrika Mashariki yatakayofanyika Kigali Rwanda Agosti mwaka Huu. (Picha na Selemani Semunyu)
………………………………………………………………………………..
Na Selemani Semunyu, JWTZ
Mkuu wa mafunzo na Utendaji 
Kivita wa Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania JWTZ Meja Jenerali 
Issa Nassoro amezitaka Timu teule za Jeshi kutobweteka na Ushindi 
wanaoupata katika mechi za majaribio wanazocheza.
Kauli hiyo imekuja Mwisho mwa 
wiki wakati  Timu ya Mpira wa Pete (Netball) Wanawake ya jeshi la 
Wananchi wa Tanzania kudhihirisha ubabe wake baada ya kuifunga Timu ya 
Mpira wa pete ya Wananume ya kikosi cha Valentia Zanzibar -KVZ kwa 
Magoli 36 kwa 24 katika mchezo uliofanyika Mwishoni mwa wiki Visiwani 
Zanzibar
Mchezo huo uliofanyika Katika 
katika uwanja wa Polisi Bwawani Ulikuwa kivutio kikubwa kutokana na 
kuhusisha jinsi mbili tofauti  kwa maana ya Wanaume na Wanawawake lakini
 pia ukiwa na wachezaji mahiri kutoka katika Timu zote mbili ambao 
wamekuwa na majina makubwa katika mchezo huo.
Meja Jenerali Nassoro aliyekuwa
 katika Ziara ya kutembelea kambi ya Timu teule za jeshi za mpira wa 
Miguu,Pete,Kikapu  na Mpira wa Mikono zilizoweka kambi katika Visiwa vya
 Unguja Mjini Zanzibar alisema ameridhishwa na kambi licha ya Jitihada 
zaidi kuongezwa ili kujihakikishia ushindi.
Alisema anamatumaini Makubwa 
historia ya kuweka kambi Zanzibar kutazibeba Timu za Jeshi kwani Timu 
mbalimbali zilizowahi kuweka kambi Zanzibar zilipata Mafanikio hivyo 
Jeshi na Taifa tunategemea hilo kama eneo zuri kwa kambi ili kujiandaa 
vizuri.
“Niliamua kwa Makusudi 
kupendekeza kambi kuwa Zanzibar nimekuwa Mchezaji na Mwanamichezo muda 
mrefu najua faida za kuweka kambi Zanzibar ukilinganisha na maeneo 
mengine kama Dar es Salaam” Alisema Meja  Jenerali Nassoro
Katika michezo ya majaribio za 
Timu hizo Teule za jeshi  Katika Mchezo wa mpira wa Kikapu Timu ya Jeshi
 wameifunga Timu ya Mbuyuni kwa Vikapu 104 kwa 58 na kuifanya Timu hiyo 
kuendeleza ubabe ikiwa ni mchezo baada ya michezo yake ya Awali 
kuzifunga Timu mabingwa wa Mchezo huo kwa Zanzibar.
Timu hizo zilizochezea kichapo 
katika Mpira wa  Kikapu  JWTZ iliifunga Stone Town kwa Vikapu 69 kwa 48 
wakati mchezo uliochezwa kabla JWTZ waliifunga polisi kwa Vikapu 68 kwa 
49 michezo iliyochezwa katika Viwanja Vya Maisara.
Katika hatua Nyingine Timu ya 
Soka ya JWTZ inakumbukumbu ya kuifunga Mafunzo kwa mabao Mawili kwa moja
 ikiwa ni mchezo wa marudiano huku mchezo wa Kwanza Timu ya Jeshi ikiwa 
imeibuka kwa Ushindi wa mabao Mawili kwa Moja, Katika mchezo Mwingine 
JWTZ wameifunga jeshi la Kujenga Uchumi JKU kwa Magoli Mawili kwa Moja.
Katika Mpira wa Mikono  JWTZ 
wameifunga Vijana Combine kwa Magoli 37 kwa 16 wakati katika Mchezo 
mwingine JWTZ waliifunga Zanzibar Warriors kwa Magoli 36 kwa 16.
 
 
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni