KOKA:AWAASA WALIMU WAKUU NA WATENDAJI KUTUNZA MADAWATI YA MISAADA
……………………………………………………………………………………………………
Na Mwamvua Mwinyi,Kibaha
MBUNGE
 wa jimbo la Mji wa Kibaha ,Silvestry Koka ,amewataka walimu wakuu wa 
shule za msingi na watendaji wa mitaa na kata katika halmashauri ya Mji 
huo, kusimamia na kuhakikisha wanayatunza madawati mapya yanayotolewa na
 wadau mbalimbali ili kuondoa tatizo la ubaha wa madawati mashuleni.
Amesema mwalimu mkuu ama mtendaji ambae atazembea kusimamia suala hilo basi atawajibishwa .
Koka
 aliyasema hayo ,wakati akikabidhi madawati 537 yenye thamani ya zaidi 
ya mil. 37 yaliyotolewa na serikali ikiwa ni mgao wa wabunge nchini 
kwenye sehemu ya posho zao .
Alieleza
 kuwa serikali haitakuwa tayari kuona madawati yanayotolewa na 
wahisani,wadau na yale yaliyotengenezwa na wadau hayafuatiliwi wala 
kupewa matunzo.
“Ni
 wajibu wa kila mtendaji,walimu na wanafunzi wenyewe kuwa wasimamizi 
kutokana na fedha zilizotumika ni kodi za wananchi hivyo lazima zilindwe
 kwa faida ya watoto hao “alisema Koka.
Aidha
 Koka alisema awali wanafunzi walikuwa wanapata shida na kero wakati wa 
kusoma ambapo wengine walikuwa wakikaa chini na kuchafuka kwa vumbi na 
kuandikia chini hivyo kushindwa kupata elimu yao kwenye mazingira yasiyo
 bora.
Alisema
 serikali ya awamu ya tano chini ya rais John Magufuli ,iliona iweke 
mkakati madhubuti wa kuchangia madawati na viti na meza katika shule za 
msingi na sekondari ili kuondoa kero ya upungufu uliokuwepo miaka ya 
nyuma.
Koka
 alisema kuwa ni jambo la lazima na sio hiari kwa walimu wakuu kuwa moja
 ya wakaguzi na wasimamizi wakuu wa madawati hayo ili hata kama yatakuwa
 yameharibika kidogo yatengenezwe na si kuyaacha hadi yaharibike .
Nae
 mwakilisha wa mkurugenzi wa halmashauri ya mji wa Kibaha Jennifer 
Omolo,afisa elimu wa halmashauri ya Mji huo,Maajabu Mkanyemka alisema 
kabla ya agizo la rais kulikuwa na mahitaji ya madawati 9,162.
Alieleza hadi kufikia June 30 walikuwa tayari wametengeneza na kukarabati madawati 6,979 hivyo kwasasa wana upungufu wa 2,183.
Maajabu
 alisema hadi sasa madawati yaliyopatikana  ni 2,500 kati ya mapungufu 
ya 2,183 huku 572 yakiwa yanatengenezwa na mara yatakapokamilika 
kutakuwa na ziada ya madawati 312 hivyo kutarajia tatizo la madawati 
kubaki historia mjini hapo.
Alisema katika upande wa shule za
 sekondari mahitaji ya meza yalikuwa 7,032 vilivyopo ni 6,041 na kubakia
 na upungufu wa meza 991 huku viti walivyokarabati na kutengeza ni viti 
6,099 kukiwa na upungufu wa viti 933 hadi sasa.
 
 
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni