Mbunge
 wa Jimbo la Ubungo Mh. Saed Kubenea akisaidiwa kujaza fomu za maombi za
 Vitambulisho vya taifa na Afisa Usajili Bi. Hadija Bauji.
Mh.
 Saed Kubenea akisaidiwa na Afisa Usajili Bw. Surera kuchukua alama za 
vidole wakati wa hatua ya uchukuaji alama za kibaiolojia.
Dr. Harrison Mwakyembe (Mb) akisaidiwa kujaza fomu na Meneja Usajili Vitambulisho vya Taifa, Bi. Julian Mafuru
…………………………………………………………………………………………..
Mamlaka ya Vitambulisho vya 
Taifa(NIDA), imeanza kusajili Waheshimiwa Wabunge wa Bunge la Jamhuri ya
 Muungano wa Tanzania; wakati wakiendelea na kikao cha Bajeti
Katika Usajili huo NIDA 
inategemea kusajili wabunge wote ambao hawakuwahi kusajiliwa awali na 
kupata vitambulisho vya Taifa, pamoja na kugawa vitambulisho
Wabunge wameonyesha mwamko mkubwa
 katika kutumia fursa hii adhimu, kwa kuhakikisha kwamba wanakuwa mstari
 wa mbele kutimiza haki yao ya kikatiba ya kusajiliwa na kupata 
kitambulisho cha Taifa; ambacho kimekuwa na faida nyingi kiuchumi, 
kijamii na kisiasa
Mpaka sasa NIDA imeshatoa zaidi 
ya  vitambulisho zaidi ya milioni 2.5 na kwa sasa NIDA iko mbioni kuanza
 usajili kwa kutumia mtaji wa taarifa toka NEC ambapo zaidi ya wananchi 
milioni 22 watasajiliwa na kupewa namba ya utambulisho ili kuanza 
matumizi mbalimbali
 
 
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni