BAYERN YABEBA KOMBE LA UJERUMANI, GUARDIOLA AMWAGA CHOZI AKIAGWA
Bayern Munich imeishinda Borussia Dortmund kwa penalti 4-3 na kubeba ubingwa wa Kombe la Ujerumani.
Huo ni ushindi wa 11 kwa Bayern kushinda makombe mawili ya Bundesliga na Kombe la Ujerumani kwa wakati mmoja.
Lakini
 klabu hiyo, imemuaga vizuri kocha Pep Guardiola ambaye alishindwa 
kujizuia na kumwaga chozi. Kocha huyo anaondoka na kwenda kujiunga na 
Manchester City.
Timu hizo zilicheza kwa dakika 120 bila kupata mshindi na zikalazimika kupigiana mikwaju ya penalti.
Kipa nyota wa Bayern, Manuel Neuer aliokoa mkwaju ya Sven Bender na Sokratis Papastathopoulos akakosa.
Kipa
 mzoefu wa Dortmund, Roman Buerki aliokoa mkwaju wa Joshua Kimmich 
lakini Thomas Muller akafunga na kuifanya Bayern iendelee kubaki kwenye 
msitari.
 








 
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni