WIZARA YA AFYA, MAENDELEO YA JAMII, JINSIA, WAZEE NA WATOTO KULAANI MAUAJI YA MTOTO SARA MGIMBA (14) WIZARA YA AFYA, MAENDELEO YA JAMII, JINSIA, WAZEE NA WATOTO YALAANI MAUAJI YA MTOTO SARA MGIMBA (14)
Wizara imesikitishwa na taarifa 
ya kifo cha mtoto Sara, ambaye mwilini wake ulioopolewa mtoni akiwa 
alitobolewa macho, mwilini akiwa mtupu; jambo linaloashiria kuwa 
marehemu alibakwa kabla ya mauti kumfika. Inaelezwa kuwa, alifungwa 
kanga shingoni, na kufungiwa ndani ya sandarusi mbili (2) zenye mawe, na
 kuzamishwa mto Lugarawa, hadi Uongozi wa kijiji cha Lugarawa walipoopoa
 mwili wake majini wakati walipoendesha msako, mapema wiki hii.  
Wizara inapongeza juhudi za 
wanakijiji na jeshi la Polisi katika mkoa wa Njombe ambao walifika 
sehemu ya tukio ili kufuatilia mauaji hayo. Ni imani ya Wizara ya watoto
 kuwa, Polisi kwa kutumia weledi wao na kwa kushirikiana na wananchi 
wataweza kuwakamata watuhumiwa wa mauaji hayo na kuwachukulia hatua 
stahiki.
Wizara inasisitiza kwamba  kila 
binadamu anayo haki ya kuishi na kupata hifadhi ya maisha yake kwa 
mujibu wa Sheria za nchi. Vitendo vya ubakaji na maujai ya kikatili 
vinapotokea katika familia zetu vinadhohofisha juhudi za wananchi katika
 kujiletea maendeleo yao ya kijamii na kiuchumi, hivyo ni muhimu kuzuia 
na kutokomeza aina zote za ukatili kwa watoto.
Wizara inaomba wanafamilia 
waliopatwa na msiba huu kuwa na moyo wa subira katika kipindi hiki cha 
majonzi makubwa, wakati Polisi wakiendelea kuwasaka watuhumiwa wa mauaji
 hayo.
                       Erasto T. Ching’oro (Msemaji)
                      Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto
                          15/4/2016
 
 
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni