ANUSURIKA KIFO BAADA YA KUJIRUSHA KUTOKA KWENYE MNARA WA SIMU JIJINI MWANZA.
Kijana Mmoja (picha) Jijini Mwanza amenusurika kifo baada yakujirusha kutoka katikati ya mnara wa simu.
Na BMG
Tukio
hilo limetokea hii leo na kuvuta watu wengi waliofika kumshuhudia
kijana huo ambae amepanda katika mnara huo tangu majira ya asubuhi na
kukatalia mnarani hadi majira ya saa sita mchana.
Mashuhuda
wa tukio hilo ambao pia ni marafiki wa karibu na kijana huyo, wamesema
huenda kijana huyo amefikia maamuzi hayo kutokana na ugumu wa maisha
ambao amekuwa akiulalamikia huku wengine wakisema ni kutokana na
kuathiriwa na matumizi ya dawa za kulevya ikiwemo gundi ambayo amekuwa
akiyatumia.
Akizungumza
kwa niaba ya Kamanda wa jeshi la uokoaji na zima moto mkoani Mwanza,
mmoja wa maafisa wa uokoaji Mussa Kaboni, amsetoa rai kwa makampuni
yenye minara ya simu kuimarisha ulinzi katika minara hiyo ili kuondoa
hatari inayoweza kujitokeza kutoka kwa raia wasio wema.
Baadhi
ya mashuhuda wa tukio hilo walionekana kuchukizwa na kitendo cha kijana
huyo na kusikika wakifoka kwa hasira na makelele ya hali ya juu “rukaa,
ruka sasa, jirushe kama wewe ni mwanaume” hali ambayo ilikuwa
ikimuongezea morari kijana huyo na hivyo kujirusha kweli kutoka katikati
ya mnara huo.
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni