MKUU WA WILAYA WETE PEMBA ALAANI VITENDO VYA HUJUMA MALI ZA WANANCHI KWA MISINGI YA KISIASA
SERIKALI ya Wilaya ya Wete Mkoa
 wa Kaskazini Pemba  imelaani  vikali  vitendo vya hujuma vinavyofanywa 
na baadhi ya wananchi kwa kuhujumu mali za wengine kwa misingi ya 
kisiasa .
Akizungumza kwa nyakati tofauti
 baada ya kutembelea maeneo yaliyohujumiwa , Mkuu wa Wilaya ya Wete 
Rashid Hadid Rashid amevitaka vyombo vya ulinzi kuhakikisha wanaohusika 
wanakamatwa na kufikishwa katika vyombo vya sheria .
Amesema serikali haitavifumbia 
macho vitendo hivyo ambavyo vinaweza kusababisha kutoweka kwa amani na 
utulivu uliopo hapa nchini .
Maeneo ambayo yamehujumiwa ni 
pamoja na bonde la Chwangayo na Mburani Shehia ya  Mtambwe kaskazini 
pamoja na Shehia ya Pembani ambapo  wakulima wamepata hasara kubwa 
kutokana na hujuma hizo.
“Serikali ya Wilaya inakilaani 
vikali kitendo hichi cha kuhujumu mali za wananchi kutokana na misingi 
ya kisiasa , tunaahidi kuwasaka wahusika wote na tutawafikisha 
mahakamani ”alieza Mkuu wa Wilaya .
Katika bonde hilo jumla ya 
mikarafuu 16 ya daraja la pili ambayo ilikuwa tayari kuzaa pamopja na 
nusu ya shamba la muhogo limehujumiwa na watu wasiojulikana.
Mmoja wa wakulima katika bonde 
hilo Bakar Mwitani Sheha amesema kuwa uharibifu katika shamba lake 
ameubaini baada ya kufika katika aneo hilo kwa ajili ya kupata mahitaji 
ya chakula.
Alisema baada ya kubaini hali 
hiyo , alitoa taarifa Ofisi ya sheha , Ofisi ya Wilaya pamoja na kutoa 
taarifa katika vyombo vya ulinzi kwa hatua zaidi .
Maeneo mengine ni shamba la 
mwakilishi wa jimbo la Mtambwe Bi Khadija Omar Kibano na Saleh Khamis 
Ahmed  ambao mashamba yao ya mpunga yamefyekwa pamoja na Said Khamis 
Mohammed na Mariam Suleiman Makame  walioharibiwa vipando vya mihogo , 
migomba , viazi , kubomolea nyumba yake pamoja na kuibwa mali ghafi 
katika kiwanda cha uchongaji huko Pembeni 
Naye  Said Khamis Mohamed wa 
Shehia ya Pembeni anayemiliki kiwanda cha kuchonga ambaye amebomolewa 
baadhi ya kuta za nyumba yake , kung’olewa vipando katika Shamba lake 
pamoja na kuchukuliwa samani (funiture) zake alisema vitendo hivyo 
vimeathiri biashara yake .
Alisema kwamba tukio hilo 
lilitokea juzi majira ya saa nane za usiku baada ya kutoka tangazo 
kupitia mskitini lililowataka wananchi wote wa Shehia hiyo kukutana , na
 baada ya hapo kundi la watu walivamia na kutekeleza hujuma hizo .
 “Nikiwa nyumbani nilisikia  tangazo likiwataka wananhi wote wa 
Shehia kukutana sokoni , na baada ya muda nilivamiwa na kundi la watu na
 kuanza kuchuma machungwa na kisha kuutaka mchungwa , kuvunja baadhi ya 
kuta katika nyumba yangu pamoja na kung’owa vipando katika shamba langu 
”alifahamisha.
 Akitoa tathmini ya hasara iliyotokea katika maeneo hayo , Afisa
 maendeleo ya Kilimo Wilaya ya Wete Makame Hamas Said alisema ni 
shilingi milioni 7,439,500 /= .
Hadi sasa hakuna mwananchi 
aliyekamatwa na vyombo vya ulinzi akihusishwa na vitendo hivyo ambapo 
jeshi la Polisi limeahidi kuwasaka na kuwafikisha mbele ya mikono ya 
sheria.
 
 
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni