TRA YAWAPA ELIMU YA MLIPAKODI WAFANYABIASHARA RAIA WA CHINA WAISHIO NCHINI TANZANIA
Meneja
wa Elimu kwa mlipa kodi kutoka TRA Bi. Diana Masalla akitoa elimu ya
mlipa kodi na sheria za kodi kwa wafanyabiashara raia wa China
wanaoishi hapa nchini na kufanya biashara katika semina ya mlipa kodi
iliyofanyika leo kwenye mgahawa wa Tang Ren Chinese jijini Dar es
salaam, ambapo kabla semina hiyo imefunguliwa na Bw. Sun Chengfeng
Mwakilishi wa masuala ya Kiuchumi na Kibiashara kutoka serikali ya Watu
wa China nchini Tanzania, Semina hiyo inalenga kuwapa wafanyabiashara
hao elimu na uelewa wa masuala mbalimbali ya kisheria katika kodi na
umuhimu wa kulipa kodi.
Baadhi
ya wafanyabiashara raia wa China wanaoishi nchini Tanzania na kufanya
biashara wakiwa katika semina ya mlipa kodi iliyofanyika leo kwenye
mgahawa wa Tang Ren Chinese jijini Dar es salaam
Bw.
Sun Chengfeng Mwakilishi wa masuala ya Kiuchumi na Kibashara kutoka
Serikali ya Watu wa China nchini Tanzania akifafanua jambo kwa waandishi
wa habari mara baada ya kufungua semina hiyo iliyofanyika kwenye
mgahawa wa Tang Ren Chinese jijini Dar es salaam.
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni