Jumatatu, 23 Mei 2016

WIZARA YA KUDHIBITI MIGOGORO YA ARDHI KWA KUFUNGUA MABARAZA YA ARDHI

nu1
Jengo la Baraza la Ardhi Kiteto.
…………………………………………………………………………………………..
Katika azma ya kuimarisha huduma ya utatuzi wa migogoro ya ardhi nchini, Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi imeendelea kuboresha na kufungua Mabaraza ya Ardhi na Nyumba ya Wilaya yatakayohusika na migogoro katika maeneo mbalimbali nchini.
Kwa upande wa Mabaraza ya Ardhi na Nyumba ya Wilaya mapya,  Baraza ambalo limeshaanzishwa rasmi, ni lile lililopo katika wilaya za Kahama na tayari limepatiwa vitendea kazi muhimu na watumishi.
Wizara imeunda Mabaraza ya Ardhi na Nyumba ya wilaya mapya 47 kupitia GN 544/2016, kati ya mabaraza hayo mapya 47, Mabaraza ya Lushoto, Kiteto, Kasulu, Kibondo na Bagamoyo yamepatiwa vitendea kazi na yataanza kufanya kazi mwishoni mwa mwaka huu wa fedha.
Aidha, uimarishaji wa Mabaraza hayo utapunguza mlundikano wa mashauri katika Mabaraza ya Ardhi na Nyumba ya Wilaya kwa kuwa migogoro isiyo ya lazima kwenda ngazi ya wilaya itasuluhishwa katika ngazi ya kijji au kata.
Katika picha ni baadhi tu ya Mabaraza ya Ardhi na Nyumba ya Wilaya ambayo yapo tayari kufunguliwa; Kiteto, Lushoto, Kigoma mjini na Kibondo.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni