WIZARA YA KUDHIBITI MIGOGORO YA ARDHI KWA KUFUNGUA MABARAZA YA ARDHI
Jengo la Baraza la Ardhi Kiteto.
…………………………………………………………………………………………..
Katika azma ya kuimarisha huduma 
ya utatuzi wa migogoro ya ardhi nchini, Wizara ya Ardhi, Nyumba na 
Maendeleo ya Makazi imeendelea kuboresha na kufungua Mabaraza ya Ardhi 
na Nyumba ya Wilaya yatakayohusika na migogoro katika maeneo mbalimbali 
nchini.
Kwa upande wa Mabaraza ya Ardhi 
na Nyumba ya Wilaya mapya,  Baraza ambalo limeshaanzishwa rasmi, ni lile
 lililopo katika wilaya za Kahama na tayari limepatiwa vitendea kazi 
muhimu na watumishi.
Wizara imeunda Mabaraza ya Ardhi 
na Nyumba ya wilaya mapya 47 kupitia GN 544/2016, kati ya mabaraza hayo 
mapya 47, Mabaraza ya Lushoto, Kiteto, Kasulu, Kibondo na Bagamoyo 
yamepatiwa vitendea kazi na yataanza kufanya kazi mwishoni mwa mwaka huu
 wa fedha.
Aidha, uimarishaji wa Mabaraza 
hayo utapunguza mlundikano wa mashauri katika Mabaraza ya Ardhi na 
Nyumba ya Wilaya kwa kuwa migogoro isiyo ya lazima kwenda ngazi ya 
wilaya itasuluhishwa katika ngazi ya kijji au kata.
Katika picha ni baadhi tu ya 
Mabaraza ya Ardhi na Nyumba ya Wilaya ambayo yapo tayari kufunguliwa; 
Kiteto, Lushoto, Kigoma mjini na Kibondo.
 
 
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni