KONGAMANO LA WADAU WA VITAMBULISHO NIDA LAFANYIKA (BOT) DAR ES SALAAM
Naibu
 Gavana wa BOT Dkt Natu Mwamba akifungua kongamano la wadau kuhusu 
vitambulisho vya Taifa lililofanyika leo katika ukumbi wa Benki Kuu na 
kuhudhuriwa na wadau toka sekta mbalimbali nchini Mkurugenzi 
 mtendaji wa Financial Sector Deepening Trust Sosthenes Kewe akichangia 
mada wakati wa kongamano wa wadau lililohusu mpango wa Usajili 
vitambulisho vya Taifa
Mkurugenzi 
 mtendaji wa Financial Sector Deepening Trust Sosthenes Kewe akichangia 
mada wakati wa kongamano wa wadau lililohusu mpango wa Usajili 
vitambulisho vya Taifa
Mr.
 Sanjay C. Rughani Makamu Mwenyekiti wa Umoja wa Mabenki Tanzania (TBA) 
na Mtendaji Mkuu wa Benki ya Standard Chartered nchini akiwasilisha mada
 wakati wa kongamano la wadau katika mpango wa usajili vitambulisho vya 
Taifa
Kaimu
 Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Vitambulisho vya Taifa Dkt. Modestus 
Kipilimba akionyesha wadau sampuli ya vitambulisho vyenye saini 
vitakavyoanza kutolewa hivi karibuni, wakati wa kongamano la wadau 
kuhusu mpango wa vitambulisho vya Taifa
Baadhi
 wa washiriki wa Kongamano la wadau kuhusu mpango wa Usajili 
vitambulisho vya Taifa wakisikiliza kwa makini mada ya mkakati wa 
Usajili kufikia Disemba 31,2016 iliyowasilishwa na NIDA
……………………………………………………………………………………………………….
Na Rose Mdami
Wadau kutoka Sekta mbalimbali 
nchini leo wamekutana katika kongamano maalumu kujadili suala la 
Vitambulisho vya Taifa na uwezekano wa kukamilika kwa mradi huo ili 
kuwezesha taifa kuwa na Kanzidata(database) yenye taarifa sahihi zenye 
kujibu maswali makuu nini ni nani, yuko wapi na anafanya nini. Lengo ni 
kurahisha utoaji huduma na kuwezesha wananchi kujishughulisha na masuala
 ya biashara kwa kuwa na mfumo rasmi unaowatambua
Akifungua kongamano hilo, Kaimu 
Gavana wa Benki Kuu ya Tanzania, Dkt. Nato Mwamba amesema mfumo wa 
Usajili na Utambuzi wa Watu ni mfumo ambao umesubiriwa kwa siku nyingi 
kwani manufaa yake ni makubwa katika mifumo mbalimbali nchini hususani 
mfumo wa biashara na taasisi za fedha nchini
Amesema kutokana na kupanuka kwa 
matumizi ya teknolojia nchini, huduma nyingi zikiwemo huduma za kifedha 
zinategemea sana kuwepo kwa mfumo wa Vitambulisho vya Taifa ili 
kuwezesha watu wengi zaidi kunufaika na huduma zitolewazo kwa sasa kwani
 wengi wanakwama kwa kuwa hakuna mfumo rasmi unaowatambua. Mafanikio ya 
mfumo huu ni kufungua milango kwa wananchi wengi zaidi kunufaika na 
huduma mbalimbali zinazoendelea kutolewa nchini zikiwemo huduma za 
kifedha na hivyo kuwataka wadau hao kuwezesha NIDA kufikia malengo ya 
usajili nchi nzima kufikia Disemba 31, 2016 ili mfumo wa Utambuzi wa 
Taifa uweze kuunganishwa na mifumo mingine
Akieleza mkakati wa usajili 
kufikia Disemba 31, 2016, Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa NIDA Dkt. Medestus 
Kipilimba amesema NIDA imejizatiti kutumia taarifa za zilizokusanywa na 
Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) kuanza usajili utakaowezesha wananchi 
waliosajiliwa katika daftari la wapiga kura kuhakikiwa na kupata usajili
 awamu ya kwanza ambao utahusisha namba ya utambulisho kabla ya kupata 
kitambulisho cha Taifa. Amesema hatua ya kufanya usajili wa awali na 
kutoa namba ya utambulisho itawezesha wananchi kuanza kufaidi 
utambulisho wao kwa kuwawezesha kupata huduma mbalimbali. Hata hivyo ili
 mwananchi kupata utambulisho kamili lazima kukamilisha hatua za usajili
 kwa kuhakikisha anawasilisha nyaraka muhimu za utambuzi ili kuendelea 
kupata huduma nyingine
Kwa mara ya kwanza NIDA itaanza 
kuzalisha vitambulisho vyenye saini ya mwombaji ambayo itawekwa kwenye 
uso wa mbele wa kitambulisho na nyumba ya kitambulisho kutakuwa na saini
 ya mtoaji. Amesema hatua zote katika kukamilisha mpango huo 
zimekamilika
Kongamano hilo limehudhuriwa na 
wadau toka Taasisi za fedha nchini, TASAF, Wamiliki wa makampuni ya simu
 nchini, Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania, Benki ya Dunia (World Bank), 
SSRA, BIMA, Melinda and Bill Gates Foundation, Tanzania Bankers 
Association( TBA) na wawakilishi wa Taasisi mbalimbali za Serikali
 
 
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni