BAJETI YA WIZARA YA MALIASILI NA UTALII YAPITISHWA, USAFIRISHAJI WA WANYAMA HAI NJE YA TANZANIA WAPIGWA MARUFUKU KWA MIAKA 3.
 Waziri
 wa Maliasili na Utalii Prof. Jumanne akijibu hoja na michango 
mbalimbali ya wabunge zilizoelekezwa kwenye wizara hiyo wakati wa 
Majumuisho ya Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara hiyo kwa mwaka 
2016/2017
ambayo imetengewa kiasi cha shilingi bilioni 135.7.
ambayo imetengewa kiasi cha shilingi bilioni 135.7.
Baadhi
 ya wabunge wakimpongeza wa Maliasili na Utalii Prof. Jumanne Maghembe 
mara baada ya Bajeti ya Wizara hiyo kupitishwa Makadirio ya Mapato na 
Matumizi ya Wizara hiyo kwa mwaka 2016/2017 ambayo
imetengewa kiasi cha shilingi bilioni 135.7.
imetengewa kiasi cha shilingi bilioni 135.7.
 Waziri
 wa Maliasili na Utalii Prof. Jumanne Maghembe akimweleza jambo Mbunge 
wa Bunda mjini Mhe. Esther Matiku (CHADEMA) nje ya ukumbi wa Bunge mara 
baada ya kupitishwa kwa Makadirio ya Mapato na Matumizi
ya Wizara hiyo kwa mwaka 2016/2017.
ya Wizara hiyo kwa mwaka 2016/2017.
 Waziri
 wa Maliasili na Utalii Prof. Jumanne Maghembe akiwa katika picha ya 
pamoja na baadhi ya Watendaji wa Wizara ya Maliasili na Utalii bungeni 
mjini Dodoma. 
 ……………………………………………………………………………………………
Na. Aron Msigwa – MAELEZO.
 Dodoma.
Serikali imesimamisha utoaji wa 
vibali na uuzaji wa wanyama hai kutoka katika hifadhi za Taifa kwenda 
nje ya Tanzania kwa kipindi cha miaka 3 mpaka hapo itakapotangazwa tena.
Waziri wa Maliasili na Utalii 
Prof. Jumanne Maghembe ametoa agizo hilo bungeni mjini Dodoma wakati 
akijibu hoja na michango mbalimbali ya wabunge iliyoelekezwa kwenye 
wizara hiyo wakati wa Majumuisho ya Makadirio ya Mapato na Matumizi ya 
Wizara hiyo kwa mwaka 2016/2017 ambayo imetengewa kiasi cha  shilingi 
bilioni 135.7.
Prof. Maghembe ameiagiza Idara ya
 Wanyamapori ipange na kuweka utaratibu mpya utakaotumika kusimamia 
biashara hiyo pindi itakaporejeshwa tena baada ya kumalizika kwa muda wa
 zuio la Serikali la miaka 3 ikizingatia  mazingira ya uhifadhi wa 
wanyama hao.
USAFIRISHAJI WA WANYAMA HAI NJE YA NCHI.
Amesema kumekuwa na taarifa za 
baadhi ya watanzania wasio waaminifu ambao wamekua wakijihusisha na 
vitendo vya kusafirisha wanyama hai waliokatazwa kinyume cha utaratibu 
jambo ambalo limeisababishia Serikali ipoteze mapato kutokana na wanyama
 hao.
Kuhusu wanyama wanaoruhusiwa 
kusafirishwa kama nyani, Kenge,ndege, kobe, wadudu na tumbili amesema 
kuwa wamekuwa wakisafirishwa  kinyume na utaratibu na baadhi ya 
wafanyabiashara wasio waaminifu kwa ajili ya kutumiwa na makampuni ya 
kimataifa kwenye shughuli za utafiti wa kisayansi wa tiba na chanjo.
Amesema makampuni hayo yamekuwa 
yakinufaika binafsi kwa kupata fedha nyingi pindi yanapofanikiwa kupata 
chanjo au tiba husika huku maeneo waliokotoka yakipata fedha kidogo 
jambo ambalo serikali ya awamu ya tano imeamua kulifanyia kazi.
 UTALII KUSINI MWA TANZANIA NA MAENEO MENGINE.
Amesema Serikali itatekeleza 
miradi mbalimbali ya uboreshaji wa Utalii wa Kusini ili kuweka mazingira
 wezeshi na kuondoa vikwazo vilivyokuwa vikisababisha watalii kushindwa 
kufika katika maeneo ya hifadhi za Taifa eneo la ukanda wa kusini  mwa 
Tanzania.
 Baadhi ya maeneo 
yatakayoshughulikiwa ni gharama ya usafiri wa ndege  kwenda na kurudi 
katika maeneo hayo kuwa kubwa hadi kufikia Dola za kimarekani 1800 jambo
 ambalo limekuwa kikwazo kwa watalii hao.
Amesema Serikali itaanzisha vituo
 vya kuwekea mafuta ya ndege mahali vilipo vivutio vya utalii ili 
kuziwezesha ndege ndogo kufika kwa urahisi na kupata huduma ya kuongeza 
mafuta ili kupunguza gharama kwa wasafiri wanaotembelea hifadhi za eneo 
hilo. 
Aidha amesema katika mwaka wa 
fedha 2016/2017 Serikali itanunua  ndege ndogo abiria ili kuwezeha 
watalii kufika kwa urahisi katika maeneo ya hifadhiza Taifa.
UTAMBUZI WA MAENEO MAPYA YA UTALII.
Serikali kwa kushirikiana na 
Wakuu wa wilaya, mikoa na Wabunge itaanzisha mpango mpya kuviorodhesha 
vivutio vyote vya utalii vilivyo katika maeneo yao ili viweze kutangazwa
 ipasavyo na kuongeza kuwa mara baada ya kukamilika kwa mpango huo 
itaandaliwa orodha ya vivutio hivyo ili vianzwe kutangazwa rasmi.
Katika kuimarisha shughuli za 
utalii nchini serikali itaweka mkazo katika uimarishaji wa utalii wa 
utamaduni, uimarishaji wa maeneo ya historia na Malikale ili kuwezesha 
eneo hilo kuchangia zaidi katika pato la taifa.
ULINZI NA USALAMA WA HIFADHI ZA TAIFA.
 Prof. Maghembe ameeleza kuwa 
suala la ulinzi na usalama wa hifadhi zote za Taifa liko kwa mujibu wa 
sheria na kubainisha kuwa serikali imeanzisha Mamlaka ya Usimamizi wa 
Wanyamapori Tanzania(TAWA) litakalochukua mbuga zote zilizokuwa na 
uongozi ambazo ziko nje ya TANAPA.
 Jeshi hilo litapambana 
kikamilifu na ujangili, kuimarisha maadili na nidhamu ya askari wa 
ulinzi wa hifadhi za taifa pamoja na kushughulikia maslahi yao na 
kuondoa migogoro kati ya askari na wananchi.
Amesisitiza kuwa mara baada ya 
Bunge la Bajeti, Wizara itakutana na wahifadhi wakuu wote ili kuweka 
vigezo vya kuzingatia katika majukumu yao na kusisitiza kuwa wahifadhi 
wote watakaoshindwa kwenda na kasi ya vigezo vilivyowekwa 
hawatajumuishwa kwenye jeshi hilo.
Aidha, amekemea vikali vitendo 
vinavyofanywa na baadhi ya askari wa hifadhi kupiga raia na kuchoma 
nyumba za wananchi kuwa havikubaliki na ni kinyume cha majukumu yao.
” Nimesikiliza kwa makini 
michango ya wabunge na nimesikia wafanyakazi katika hifadhi zetu 
wanapiga raia wanaua mifugo na kuchoma nyumba za wananchi jambo ambalo 
halikubaliki, hatukuwatuma kufanya hivyo” Amesisitiza Prof.Maghembe.
MIGOGORO YA MIPAKA MAENEO YA HIFADHI.
Serikali imesema mpaka sasa kuna 
migogoro ya ardhi 281, kati ya hiyo 35 ambayo ni sawa na asilimia 12.5 
ni migogoro ya hifadhi na kuita  Mikoa yenye migogoro hiyo kuwa ni 
pamoja na Mara , Tanga na Kagera inachukua jumla ya asilimia 50.
Aidha, amesema kuwa mkoa wa 
Tabora unaongoza kwa kuwa na eneo kubwa la ardhi na unaongoza kwa kuwa 
na migogoro mingi ya hifadhi kwa asilimia 40.
Katika kuishughulikia migogoro 
hiyo Serikali imeziagiza wizara za Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi,
 Maji na Umwagiliaji, TAMISEMI, Nishati na Madini, Ofisi ya Makamu wa 
Rais – Mazingira pamoja na Wizara ya Maliasili na Utalii kushirikiana 
pamoja katika kutatua migogoro yote ya ardhi nchini.
UBORESHAJI WA MAENEO YA HIFADHI NA MAMLAKA ZA UHIFADHI.
 Amesema katika mwaka wa fedha wa
 2016/2017 kiasi cha shilingi bilioni 1 kimetengwa kushughulikia usafi 
wa mazingira na ujenzi wa vyoo vya kisasa  katika hifadhi ya mlima 
Kilimanjaro vitakavyokuwa na uwezo wa kugeuza maji taka kuwa poda ili 
kuweka mazingira yote ya mlima huo kuwa safi.
Aidha,amesema kuwa Mamlaka za 
hifadhi za Taifa zimeendelea kuchangia katika maendeleo ya wananchi 
katika maeneo mbalimbali nchini ikiwemo ujenzi wa madarasa, miundombinu 
ya barabara, utoaji wa madawati katika halmashauri mbalimbali nchini.
 




 
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni