Alhamisi, 26 Mei 2016

Maliasili na Tamisemi wasaini mkataba wa makubaliano uendelezaji misitu

index1
Baadhi ya wajumbe wakiwa katika mkutano huo
index2 
Wizara ya maliasili na utalii kupitia wakala wa huduma za misitu leo wamesaini mkataba wa makubaliano kuhusu ushirikiano wa uendelezaji misitu na wizara ya TAMISEMI.
Maeneo ya kuzingatia katika mkataba huo yametajwa kuwa ni kuimarisha ushirikiano katika Misitu  na utawala bora, uperembaji miradi inayofadhiliwa na mfuko wa misitu Tanzania pamoja na kuboresha ukusanyaji, ugawaji, utumiaji na ufuatiliaji wa matumizi ya asilimia 5 ya tuzo za upandaji miti.
Awali kabla ya kusaini mkataba wa makubaliano katibu mkuu wa wizara ya maliasili na utalii Meja Jenerali Gaudence Milanzi alisema wizara yake inalenga kuimarisha utendaji wake hivyo aliwaagiza watendaji kusimamia misingi ya mkataba huo wa makubaliano katika utekelezaji wa majukumu ili kufikia malengo yaliyokusudiwa.
Kwa upande wake Katibu Mkuu TAMISEMI Injinia  Musa Iyombe ambaye amewakilishwa na Bw. Mohamed Pagawa aliwataka Maafisa Misitu kufanya kazi kwa ushirikiano kama Mkataba Unavyotaka lakini pia kuzingatia sheria, kanuni na Utaratibu katika uendelezaji wa Rasilimali Misitu
Mkurugenzi wa Mipango na Matumizi ya Rasilimali Misitu Bw. Mohamed Kilongo akitoa ufafanuzi kuhusu makubaliano hayo amesema tathmini ya Rasilimali Misitu inakabiliwa na changamoto kuu mbili na amezitaja kuwa ni uharibifu Mkubwa wa Misitu unaofikia kiasi cha hekta 372,000 kwa mwaka na mahitaji ya mazao ya misitu kwa mwaka yanazidi uwezo wa Misitu kwa zaidi ya Meta za ujazo Milioni 19.5.
Amesema ili kukabiliana na changamoto hizo kunahitajika jitihada za pamoja kuboresha usimamizi wa rasilimali za misitu na kupunguza uharibifu katika hifadhi zetu. Kazi kubwa iliyopo mbele yetu ni kupanda miti hekta 185,000/= kwa mwaka kwa ajili ya kukidhi mahitaji ya Mazao ya Misitu.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni