Maliasili na Tamisemi wasaini mkataba wa makubaliano uendelezaji misitu
Baadhi ya wajumbe wakiwa katika mkutano huo
Wizara
 ya maliasili na utalii kupitia wakala wa huduma za misitu leo wamesaini
 mkataba wa makubaliano kuhusu ushirikiano wa uendelezaji misitu na 
wizara ya TAMISEMI.
Maeneo ya kuzingatia 
katika mkataba huo yametajwa kuwa ni kuimarisha ushirikiano katika 
Misitu  na utawala bora, uperembaji miradi inayofadhiliwa na mfuko wa 
misitu Tanzania pamoja na kuboresha ukusanyaji, ugawaji, utumiaji na 
ufuatiliaji wa matumizi ya asilimia 5 ya tuzo za upandaji miti.
Awali kabla ya kusaini 
mkataba wa makubaliano katibu mkuu wa wizara ya maliasili na utalii Meja
 Jenerali Gaudence Milanzi alisema wizara yake inalenga kuimarisha 
utendaji wake hivyo aliwaagiza watendaji kusimamia misingi ya mkataba 
huo wa makubaliano katika utekelezaji wa majukumu ili kufikia malengo 
yaliyokusudiwa.
Kwa upande wake Katibu 
Mkuu TAMISEMI Injinia  Musa Iyombe ambaye amewakilishwa na Bw. Mohamed 
Pagawa aliwataka Maafisa Misitu kufanya kazi kwa ushirikiano kama 
Mkataba Unavyotaka lakini pia kuzingatia sheria, kanuni na Utaratibu 
katika uendelezaji wa Rasilimali Misitu
Mkurugenzi wa Mipango 
na Matumizi ya Rasilimali Misitu Bw. Mohamed Kilongo akitoa ufafanuzi 
kuhusu makubaliano hayo amesema tathmini ya Rasilimali Misitu 
inakabiliwa na changamoto kuu mbili na amezitaja kuwa ni uharibifu 
Mkubwa wa Misitu unaofikia kiasi cha hekta 372,000 kwa mwaka na mahitaji
 ya mazao ya misitu kwa mwaka yanazidi uwezo wa Misitu kwa zaidi ya Meta
 za ujazo Milioni 19.5.
Amesema ili kukabiliana
 na changamoto hizo kunahitajika jitihada za pamoja kuboresha usimamizi 
wa rasilimali za misitu na kupunguza uharibifu katika hifadhi zetu. Kazi
 kubwa iliyopo mbele yetu ni kupanda miti hekta 185,000/= kwa mwaka kwa 
ajili ya kukidhi mahitaji ya Mazao ya Misitu.
 
 
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni