Idadi ya vifo kwa watoto wachanga na wakina mama vyazidi kupungua Nchini.
Balozi
 wa Ujerumani Mhe. Egon Kochanke akiongea na waandishi wa habari na 
Wadau wa Mpango wa Tanzania na Ujerumani kusaidia Afya (TGPSH) hawapo 
pichani wakati wa ufunguzi wa maonesho ya picha yanayofanyika Makumbusho
 ya Taifa mpaka Juni 10 mwaka huu jijini Dar es salaam.
Mwakilishi
 wa Katibu Mkuu Wizara ya Afya , maendeleo ya Jamii , Jinsia na Watoto ,
 Mkurugenzi wa Tiba Dkt. Margaret Mbando akiongea na waandishi wa habari
 na Wadau wa Mpango wa Tanzania na Ujerumani kusaidia Afya (TGPSH) 
hawapo pichani wakati wa ufunguzi wa maonesho ya picha yanayofanyika 
Makumbusho ya Taifa mpaka Juni 10 mwaka huu jijini Dar es salaam.
Balozi
 wa Ujerumani Mhe. Egon Kochanke  kulia akikata utepe kuashilia kuanza 
rasmi kwa maonesho ya picha yanayofanyika Makumbusho ya Taifa mpaka Juni
 10 mwaka huu jijini Dar es salaam na wa kwanza kushoto ni Mwakilishi wa
 Katibu Mkuu Wizara ya Afya , maendeleo ya Jamii , Jinsia na Watoto , 
Mkurugenzi wa Tiba Dkt. Margaret Mbando.
Mshauri
 wa ufundi kutoka Mpango wa Tanzania na Ujerumani kusaidia Afya (TGPSH) 
Dkt. Baltazar Ngoli wa kwanza kulia  akitoa maelekezo ya picha kwa 
Balozi wa Ujerumani Mhe. Egon Kochanke  wa pili kulia pamoja na 
Mwakilishi wa Katibu Mkuu Wizara ya Afya , maendeleo ya Jamii , Jinsia 
na Watoto , Mkurugenzi wa Tiba Dkt. Margaret Mbando  wa tatu kulia 
wakati wa ufunguzi wa  maonesho ya picha yanayofanyika Makumbusho ya 
Taifa jijini Dar es salaam.
Wadau
 mbalimbali wa Mpango wa Tanzania na Ujerumani kusaidia Afya (TGPSH) 
wakifuatilia kwa makini maelezo ya Mwakilishi wa Katibu Mkuu Wizara ya 
Afya , maendeleo ya Jamii , Jinsia na Watoto , Mkurugenzi wa Tiba Dkt. 
Margaret Mbando hayupo  pichani wakati wa ufunguzi wa maonesho ya picha 
yanayofanyika Makumbusho ya Taifa mpaka Juni 10 mwaka huu jijini Dar es 
salaam.
Idadi ya vifo kwa watoto wachanga na wakina mama vinazidi kupungua kutoka siku hadi siku katika kufikia malengo ya milenia .
Akizungumza hayo katika hafla 
fupi ya kuzindua maonesho ya picha Mwakilishi wa Katibu Mkuu Wizara ya 
Afya , maendeleo ya Jamii , Jinsia na Watoto , Mkurugenzi wa Tiba Dkt. 
Margaret Mbando amesema kuwa Tanzania imepiga hatua katika kufikia 
malengo ya milenia kwa kupunguza Idadi ya vifo kwa watoto wachanga na 
wakina mama.
“Tumefanikiwa kupunguza Idadi ya 
vifo kwa watoto wachanga na wakina mama ili kufikia malengo ya milenia 
kwa upande wa afya kupitia mfumo wa kujiunga na bima ya afya kwa jamii” 
alisema Dkt. Mbando.
Mbali na hayo Dkt Mbando amesema 
kuwa amewakaribisha wananchi wote hususani wakazi wa Dar es salaam 
kuudhuria maonesho hayo yaliyofunguliwa leo yenye kauli mbiu ya “Huduma 
Bora kwa Afya Bora”yatayofikia kilele mpaka Juni 10 mwaka huu ili kupata
 ujumbe zaidi kupitia picha yanayofanyika Makumbusho ya Taifa jijini.
Aidha ameipongeza Serikali ya 
Ujerumani kupitia ubalozi wake kwa kushirikiana vizuri na Serikali ya 
Tanzania na kukubaliana  kupata msaada wa Euro milioni 47 kwa muda wa 
miaka mitatu ijayo katika kuinua sekta ya Afya.
Kwa upande wa balozi wa Ujerumani
 Mhe. Egon Kochanke amesema kuwa mchango wa Serikali ya ujerumani kwa 
sekta ya afya Tanzania utaendelea kuwa sehemu ya mpango wa ushirikiano 
wa nchi mbili ili kuinua sekta hiyo nchini.
 
 
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni