Mshindi wa bahati nasibu ya Taifa kupatikana kesho
Mbunge
 wa zamani jimbo la Nanyumbu Dastan Mkapa (kulia) akipewa maelezo namna 
mshindi wa  bahati nasibu ya Taifa atakavyopatikana mara baada ya kukata
 tiketi ya mchezo huo katika viwanja vya Nyerere Square mjini Dodoma 
jana baada ya kuzinduliwa rasmi ukataji tiketi za mchezo.
Wakala
 wa ukataji tiketi za mchezo wa bahati nasibu ya Taifa  mjini Dodoma 
Jamila Baduwel akitoa huduma hiyo kwa mmoja wa wananchi aliyetaka 
kununua tiketi za kushiriki.
…………………………………………………………………………………………………
Na Mwandishi wetu
Baada
 ya  kampuni ya Murhandizwa kutoka nchini Afrika ya Kusini ambayo 
ilipewa leseni ya kuendesha mchezo wa bahati nasibu ya taifa kuanza 
kuuza tiketi za mchezo huo wiki iliyopita ,leo (Jumamosi) ndio mchezo wa
 kwanza utafanyika na mshindi wa kitita cha shilingi milioni 100  
atatangazwa.
Mwenyekiti
 wa kampuni ya Gidani International ambayo ni kampuni mama ya kampuni ya
 Murhandizwa,Prof .Bhongani Khumalo alisema kuwa michezo yote 
itaendeshwa kwa utaalamu  kwa kutumia teknolojia ya kisasa na kwa  uwazi
 vilevile  kuanza kwa mchezo huo hapa nchini ni mwendelezo wa michezo 
mingine mingi ya bahati nasibu itakayokuja baadaye.
“Kampuni
 yetu inao uzoefu wa muda mrefu kuendesha michezo ya Bahati Nasibu na 
tutahahakikisha watanzania  wananufaika na mchezo huu pia tutachangia 
pato la taifa kwa njia ya kodi kupitia mchezo huu.Aliongeza kuwa  
uchezeshaji wa mchezo utakuwa wa wazi kupitia vyombo vya habari na 
mshindi atakuwa anatangazwa na kupatiwa fedha zake mara moja bila kuwepo
 urasimu wa aina yoyote.
Kwa
 upande wake Mkurugenzi Mkuu wa Bodi ya Michezo ya Kubatisha ya 
Taifa,Abbas Tarimba aliwataka watanzania kuchangamkia fursa hii kwa 
kununua tiketi za kushiriki katika mchezo kutoka kwa mawakala 
waliosambaa nchini kote ili waweze kujishindia zawadi ya mamilioni ya 
fedha na kubadilisha maisha yao.
Tarimba
 aliwataka wananchi wasiwe na hofu ya kushiriki kwenye mchezo kwa kuwa 
unafanyika kwa kufuata kanuni na taratibu zilizowekwa na serikali 
“Wananchi wasiwe na wasiwasi kushiriki kwenye mchezo huu kwa kuwa fedha 
zao na kanuni za uendeshaji wa mchezo vinasimamiwa na serikali.
Alisema
 ujio wa mchezo huu nchini mbali na kuwanufaisha  washindi binafsi 
utachangia kupanue wigo wa ajira kwa Watanzania wengi watakaosimamia 
zoezi la ukatishaji tiketi katika vituo zaidi 20,000 vitakavyofunguliwa 
Nchi nzima.
Tiketi
 za mchezo huu zimeanza kuuzwa nchi nzima na wakati wa uzinduzi wa 
huduma za kampuni mkoani Dodoma wananchi wengi walijitokeza kununua 
tiketi za kushiriki na walishauri mtandao wa kuuza tiketi ufanyike 
kupitia hata kwenye simu za mkononi ili kuwawezesha wananchi wengi 
kushiriki kununua tiketi ambayo kila moja inauzwa shilingi 500/-
 
 
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni