SERIKALI KUMLINDA MKULIMA KWA KUANZISHA VITUO VYA UNUNUZI WA MAZAO.
Wakala wa Vipimo kwa 
kushirikiana na Mamlaka ya Serikali za Mitaa inakusudia kuanzisha  vituo
 maalum vya ununuzi wa mazao ya wakulima (buying centres) katika 
vitongoji nchi nzima ili kuondoa unyonyaji na ukandamizaji unaofanwa na 
wachuuzi wa mazao ya wakulima.
Kauli hiyo imetolewa leo mjini 
Dodoma na Waziri wa Viwanda,Biashara na Uwekezaji Mhe. Charles Mwijage 
wakati akijibu swali la Mbunge wa Mlalo Mhe. Rashid Shangazi aliyetaka 
kujua ni lini Serikali itasimamia sheria kuondoa unyonyaji unaofanywa na
 wachuuzi wakati wa kununua mazao ya wakulima.
Alisema kuwa katika kutekeza 
hayo hakuna mfanyabiashara atakayeruhusiwa kusafirisha mazao ambayo 
yamefungashwa kinyume kinyume cha Sheria ya vipimo na kuongeza kuwa 
katika kusimamia jambo hilo vitaanzishwa vituo maalum vya ukaguzi bila 
kusabaisha usumbufu katika ufanyaji biashara.
Mhe. Mwijage amewaagiza Maafisa
 Ugani walioko vijijini watumike kusimamia matumizi ya vipimo rasmi 
katika vituo hivyo na kutoa taarifa zote muhimu kwa Wakala wa Vipimo.
Aidha ,alisema kuwa Serikali 
imeamua kufanyia mapitio Sheria ya Vipimo sura 340 ili kuondokana na 
unyonyaji na ukandamizaji unaofanywa na wachuuzi wa mazao ya wakulima.
Alisema kuwa Serikali imeamua 
kufanyia mapitio ya Sheria hiyo ili kuweka mazingira mazuri kwa lengo la
 kumlinda muuzaji kwa kuwadhibiti manunuzi wanaotumia njia za 
udandanyifu wakati wanaponunua mazao ya wakulima.
Mhe. Mwijage alisema kuwa 
katika kipindi kifupi kijacho Serikali itawalisha mabadiliko hayo 
bungeni ili ifanyiwe marekebisho yanayostahili.
Aidha , Waziri huyo alisema 
kuwa pamoja na marekebisho ya Sheria ya Vipimo yanatarajia kufanywa , 
Wakala wa Vipimo imewasilisha Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali 
za Mitaa (TAMISEMI) mapendekezo ya kutungwa kwa sheria ndogo(by laws)  
ili ziweze kuwaongoza wakulima na wafanyabiashara kufungasha mazao.
 
 
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni