ESRF yafanya warsha kujadili Mpango wa Maendeleo Endelevu (SDG)
Na Rabi Hume, Modewjiblog
Katika
 kusaidia kukamilika kwa Mpango wa Maendeleo Endelevu ambao unataraji 
kumalizika 2030, Taasisi ya Utafiti wa Uchumi na Kijamii (ESRF) imefanya
 warsha ambayo imekutanisha wadau mbalimbali ili kuona ni jinsi gani 
wanaweza kubadilishana mawazo ili kufanikisha mpango huo nchini.
Mgeni
 rasmi katika warsha hiyo alikuwa ni Mkurugenzi wa Kupunguza Umaskini na
 Kuinua Uchumi kutoka Wizara ya Fedha, Anna Mwasha ambaye wakati 
akifungua warsha hiyo alisema kuwa mpango huo ni muhiu wa nchi yetu kwa 
sababu unakwenda kubadili maisha ya kila Mtanzania ili kuondokana na 
umaskini na kuwa katika maisha bora kama jinsi malengo 17 ya mpango huo 
yanavyojieleza.
Mo 
Dewji Blog ilipata nafasi ya kuhudhuria mkutano huo na kukuandalia 
habaroi picha jinsi warsha hivyo ilivyofanyika katika ukumbi wa ESRF.
Mkurugenzi
 Mtendaji wa Taasisi ya Utafiti wa Uchumi na Kijamii (ESRF), Dkt. Tausi 
Kida akitoa neno la ufunguzi katika warsa iliyoandaliwa na ESRF ili 
kuzungumzia Mpango wa Mendeleo Endelevu (SDG). (Picha zote na Rabi Hume,
 Modewjiblog)
Baadhi
 ya washiriki waliohudhuria warsha hiyo wakimsikiliza kwa makini 
Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Utafiti wa Uchumi na Kijamii, Dkt. 
Tausi Kida wakati akifungua warsha hiyo.
Mkurugenzi
 Mkazi wa Shirika la Umoja wa Mataifa la Maendeleo (UNDP), Awa Dabo 
akitoa neno kwa niaba ya UNDP ambao ndiyo wasimamizi wa mpango huo. 
Kulia ni Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Utafiti wa Uchumi na Kijamii 
(ESRF), Dkt. Tausi Kida na Mkurugenzi wa Kupunguza Umaskini na Kuinua 
Uchumi kutoka Wizara ya Fedha, Anna Mwasha 
Mgeni
 rasmi katika warsha hiyo, Mkurugenzi wa Kupunguza Umaskini na Kuinua 
Uchumi kutoka Wizara ya Fedha, Anna Mwasha akifungua warsha hiyo 
iliyoandaliwa na Taasisi ya Utafiti wa Uchumi na Kijamii (ESRF).
Washiriki wakiendelea kufatilia kinachoendelea katika warsha hiyo.
Stephen Chacha kutoka Shirika la Beyond 2015 for Africa akizungumza jinsi Mpango wa SDG unaweza kufanyika nchini.
Mmoja wa washiriki, Dkt. Kitila Mkumbo akichangia mada zilizokuwa zikijadiliwa.
Washiriki wakiwa katika picha ya pamoja.
 
 
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni