TAKUKURU yawahamasisha wananchi kushishiriki kampeni ya LONGA NASI
Kaimu
 Mkuu wa Sehemu ya Uratibu na utoaji Habari,Idara ya Elimu kwa Umma toka
 Taasisi ya Kuzuia na Kupmbana na Rushwa (TAKUKURU) Bw. Matai Kirumbi  
akizungumza na waandishi wa habari  leo Jijini Dar es salaa kuhusu faida
 za kampeni ya LONGA NASI iliyozinduliwa na Taasisi hiyo hivi karibuni 
ikilenga kuhamasisha wananchi kushiriki vita dhidi ya rushwa kwa 
kuwafichua wale wote wanaojihusisha na vitendo hivyo. Kushoto ni Afisa 
Uhusiano nwa Taasisi hiyo Bi Angela Mulanduzi.
…………………………………………………………………………………………………………….
Frank Mvungi – MAELEZO
TAKUKURU yawahamasisha wananchi  kushishiriki kampeni ya LONGA NASI  ili kukomesha vitendo vya rushwa hapa nchini.
Kauli hiyo imetolewa leo Jijini 
Dar es Salaam na Kaimu Mkuu wa Sehemu ya Uratibu na utoaji Habari,Idara 
ya Elimu kwa Umma toka Taasisi ya Kuzuia na Kupmbana na rushwa 
(TAKUKURU) Bw. Matai Kirumbi wakati wa mkutano na vyombo vya Habari.
Akizungumzia Kampeni hiyo, 
 Kirumbi amesema inalenga kuwajengea uelewa wananchi kuhusu mapambano 
dhidi ya rushwa ili kuzuia vitendo vya rushwa .
Katika Kampeni hiyo wananchi 
wanatakiwa kutoa taarifa za kuwepo kwa vitendo vya rushwa au viashiria 
vyake kwa kupiga namba 113 au *113# kupitia simu  ya kiganjani .
Huduma hiyo  inapatikana kupitia mitandao ya AIRTEL,TIGO,HALOTEL,VODACOM na  ZANTEL ambapo wananchi hawatatozwa gharama yoyote.
“Taarifa 8000 zimeshapokelewa na 
Taasisi yetu tangu kuzinduliwa kwa Kampeni hii na nyingi ni za wananchi 
kuombwa hongo na tayari tunazifanyia kazi “alisisitiza Kirumbi.
Akifafanua kuhusu taarifa hizo 
Kirumbi amesema kuwa zinaonyesha wananchi wamepokea vizuri kamapeni hiyo
 iliyozinduliwa tarehe 24/5/2016 na Makamu wa Rais Mh. Samia Suluhu 
Hassan.
Katika kampeni hiyo wananchi 
watajengewa ujasiri zaidi ili kuongeza ushiriki wao katika mapambano 
dhidi ya rushwa kwa kutoa taarifa na kutoa mrejesho wa kero 
zilizotatuliwa.
Matarajio ni kuongezeka kwa ubora
 wa huduma za jamii kwa kuwa fedha za umma zitatumika kama ilivyopangwa 
katika huduma kama vile kununua dawa.
Akizindua kampeni ya LONGA NASI 
jumanne tarehe 24,Mei 2016 katika viwanja vya Mwembeyanga Wilayani 
Temeke Jijini Dar es Salaam, Makamu wa Rais, Mh. Samia Suluhu Hassan 
alisisitiza suala la ushiriki wa kila mmoja katika mapambano dhidi ya 
rushwa nchini alisema”Tunahitaji nguvu za pamoja ili kumaliza tatizo la 
rushwa nchini”.
 
 
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni