Alhamisi, 19 Mei 2016

BREAKING NEWS- NDEGE YA MISRI YAPOTEA IKIWA NA ABIRIA 59 IKITOKA PARIS

4bk3658505242c5fuv_620C350 BBtdVkw 
Ndege moja ya shirika la ndege la Misri la EgyptAir, iliyokuwa ikitoka mji mkuu wa Ufaransa Paris hadi Cairo, imepotea kutoka kwenye mitambo ya rada.
Maafisa wanaosimamia safari za ndege wanasema kuwa ndege hiyo aina ya Airbus A320, ilikuwa na abiria 59 na wahudumu kumi.
Shirika hilo limesema kuwa ndege hiyo ilitoweka katika maeneo ya mashariki ya bahari ya Mediterranean, kilomita 16 kabla ya kufika katika anga ya Misri.
Misri imetuma ndege za kivita kusaka ndege hiyo kwa ushirikiano na utawala wa Ugiriki.
 
Picha kwa hisani ya msm

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni