Jamii yatakiwa kudumisha na kuenzi Utamaduni
Kaimu
 Mkurugenzi  Idara ya Utamaduni Bi. Lily Beleko  kutoka Wizara ya 
Habari,Utamaduni,Sanaa na Michezo akisikiliza swali kutoka kwa mwandishi
 wa habari  (hayupo pichani) wakati alipokuwa akizungumza na waandishi 
wa habari  kuhusu maadhimisho ya siku ya Uanuwai wa Utamaduni 
yanayotarajia kufanyika  Mei 21 mwaka huu.Picha na Eliphace Marwa – 
MEELEZO
Kaimu
 Mkurugenzi  Idara ya Utamaduni Bi. Lily Beleko  kutoka Wizara ya 
Habari,Utamaduni,Sanaa na Michezo akisisitiza jambo wakati alipokuwa 
akizungumza na waandishi wa habari (hawapo pichani) kuhusu maadhimisho 
ya siku ya Uanuwai wa Utamaduni yanayotarajia kufanyika  Mei 21 mwaka 
huu ,kulia ni Afisa Habari  wa Wizara hiyo Bw.Benjamini Sawe.
Katika kuelekea kilele cha 
maadhimisho ya siku ya Uanuwai wa  Utamaduni Duniani Serikali imeitaka 
jamii kuhifadhi kulinda na kuheshimu utamaduni wa nchi kwa vile ndio 
kitambulisho cha Taifa letu ili kuweza kutambulika ndani na nje ya nchi.
Wito huo umetolewa leo Jijini Dar
 es Salaam na Kaimu Mkurugenzi wa Idara ya Utamaduni kutoka Wizara ya 
Habari,utamadunu,Sanaa na Michezo  Bi.Lily Beleko wakati akizungumza na 
Waandishi wa habari kuhusu cha maadhimisho ya siku ya Uanuwai wa  
Utamaduni Duniani ambapo kauli mbiu ya madhimisho ya mwaka huu ni” 
Utamaduni wa Uadilifu na Nidhamu ya Kazi Huleta Maendeleo”, “Sasa Kazi  
Tu”.
Kaimu Mkurugenzi wa Utamaduni 
Bi.Lily Beleko amesema kuwa ni wajibu kwa kila  mtanzania kuheshimu  
Utamaduni wetu na kushiriki kikamilifu katika  kuutambua, kuujenga, 
kuuendeleza  na kuurithisha kwa vizazi vingine.
“Siku hii ni maalumu kwa kila 
mtanzaniana na kila mmoja hana budi kukubaliana na harakati hizi za 
kulinda, kuhifadhi na kuendeleza Utamaduni wetu kwa ajili ya vizazi 
vijavyo”Alisema Bi Lily.
Bi.Lily Beleko ameongeza kuwa  
nchi haiwezi kutambulika na kuheshimika  kama Taifa huru bila kuwa na 
Utamaduni wake hivyo kuwepo kwa maadhimisho haya kunaipatia jamii fursa 
ya kuendelea kukumbushana ,kuhamasishana na kuhimizana katika kuuenzi 
utamaduni wa nchi.
Siku ya Uanuwai wa Utamaduni 
Duniani huadhimishwa kila ifikapo tarehe 21 Mei, ambapo siku hiyo 
imeteuliwa na  Baraza kuu la Umoja wa Mataifa kuona umuhimu wa kuhifadhi
 na kuendeleza Utamaduni na hivyo kupitisha Azimio Na 57/249 mnamo mwaka
 2002.
 
 
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni