Mtanzania ashinda tuzo kubwa ya kampuni ya SABMiller
 Bundala AlexSemamba akiwa na  Mkurugenzi wa SABMiller wa kanda ya Afrika,Mark Bowman
na wafanyakazi wenzake kutoka nchi mbalimbali wakati wa hafla ya kutumiwa tuzo.
na wafanyakazi wenzake kutoka nchi mbalimbali wakati wa hafla ya kutumiwa tuzo.
Bundala Alex Semamba akiwa wafanyakazi  wenzake kutoka nchi mbalimbali wakati wa hafla ya kutumiwa tuzo.
……………………………………………………………….
 Na Mwandishi wetu
Meneja Uendeshaji wa kampuni ya konyagi Bundala Alex Samamba ametunikiwa tuzo kubwa
inayojulikana kama SABMiller Africa Master,tuzo inayotolewa kwa wafanyakazi wa muda
mrefu na waliotoa mchango wa pekee kuendeleza kampuni na ni moja ya tuzo kubwa na inayoheshimika kwa kampuni hiyo.
inayojulikana kama SABMiller Africa Master,tuzo inayotolewa kwa wafanyakazi wa muda
mrefu na waliotoa mchango wa pekee kuendeleza kampuni na ni moja ya tuzo kubwa na inayoheshimika kwa kampuni hiyo.
Hafla
 ya kutunukiwa tuzo hiyo ilifanyika katika mkutano maalumu wa maafisa 
mauzo na masoko wa kampuni ya SABMiller uliofanyika mjini Cape Town 
nchini Afrika ya Kusini wiki iliyopita na alitunikiwa tuzo hiyo na 
Mkurugenzi wa SABMiller wa
kanda ya Afrika,Mark Bowman akiwa ni mtanzania peke yake na mfanyakazi wa kwanza wa kampuni ya Konyagi kuipata.
kanda ya Afrika,Mark Bowman akiwa ni mtanzania peke yake na mfanyakazi wa kwanza wa kampuni ya Konyagi kuipata.
Akiongea
 muda mfupi baada ya kupata tuzo hiyo Bundala alisema kuwa anawashukuru 
wafanyakazi wenzake wote ambao akifanya kazi nao kwa ushirikiano kwa 
kuwa mafanikio mara  nyingi yanapatikana kutokana na kufanya kazi kwa 
bidii na
kwa ushirikiano.
kwa ushirikiano.
“Tuzo
 hii japo nimetunukiwa mimi lakini ni kwa ajili ya wafanyakazi wote wa 
kampuni ya Konyagi ambao nimekuwa nikifanya nao kazi kila siku na 
kukabiliana a changamoto  mbalimbali za ushindani zilizopo katika masoko
 kwa sasa”.Alisema
Anakumbuka
 safari mbalimbali alizopitia katika kazi za mauzo ambazo anaeleza kuwa 
zinahitaji kuwa mtu mwenye bidii ya kazi na kufanyika  kazi ushauri wa 
wateja “Pamoja na elimu na nyadhifa nilizoshikilia nilipokuwa kwenye  
kazi za usambazaji nilikuwa nafanya kazi pia ya udereva wa malori 
makubwa ya kufikisha bidhaa kwa wateja na wakati mwingine kulazimika  
kupakua mzigo”.Anasema Alex
Bundala
 alijiunga na kampuni ya Konyagi miaka 22 iliyopita katika Idara ya 
mauzo na Masoko na kutokana na bidi katika kazi aliweza kupandishwa cheo
 kuwa Meneja Masoko na Mauzo anayesimamia kanda mbalimbali.
Kutokana na umahiri wake katika ubunifu wa mauzo na uendelezaji wa masoko alipandishwa Cheo
kuwa Meneja wa kuendeleza Masoko wa kampuni ambapo baadaye aliteuliwa kushika nafasi aliyonayo kwa sasa hivi ya Meneja Uendeshaji wa kampuni.
kuwa Meneja wa kuendeleza Masoko wa kampuni ambapo baadaye aliteuliwa kushika nafasi aliyonayo kwa sasa hivi ya Meneja Uendeshaji wa kampuni.
 



 
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni