Tapeli wa madini akamatwa Dar
Kamanda
 wa Polisi kanda maaalum ya Dar es Salaam Kamishna Simon Sirro akionesha
 waandishi wa habari mzani unaodaiwa kutumiwa na tapeli wa madini kupima
 madini bandia na kuwatapeli wananchi wakati wa kutoa taarifa ya 
kukamatwa kwa tapeli huyo Jijini Dar es salaam Mei 20 2016.
Jeshi la Polisi Kanda Maalum ya 
Dar es Salaam limemkamata mtuhumiwa anayejulika kwa jina la Wenceslaus 
Mtui(46) mkazi wa Makongo Juu kwa kosa la utapeli wa sh. Milioni 90 .
Akizungumza na waandishi wa 
habari leo Jijini Dar es Salaam Kamanda wa Polisi kanda maaalum ya Dar 
es Salaam Kamishna Simon Sirro amesema wamefanikiwa kumkamata tapeli 
huyo mara baada ya kupata taarifa kutoka kwa Bw. Kelvin Nyerere(26) 
mkazi wa Msasani ambaye alishawishiwa na kutapeliwa kwa kuuziwa madini 
bandia na mtuhumiwa huyo.
Kwa mujibu wa kamanda Sirro, 
mtuhumiwa huyo alikamatwa mara baada ya kupata taarifa kutoka kwa 
Nyerere aliyetapeliwa, askari walifika eneo la tukio na kumkamata 
mtuhumiwa  na kumfikisha kituo cha polisi kwa mahojiano.
Aidha baada ya kufanyika kwa 
upekuzi ofisini na nyumbani kwa mtuhumiwa, kulikutwa na vitu 
vilivyodhaniwa kuwa ni madini, chuma cha kuchomea madini, mashine ya 
kupimia madini, vifaa vya kubania madini (53), mashine ya kupimia 
madini, nyaraka za kuwekea fedha kutoka Benki mbalimbali na hati za 
usajili wa makampuni ambazo zilitiliwa shaka.Vielelezo vyote 
vilichukuliwa kwa uchunguzi.
Mtuhumiwa huyo bado anashikiliwa 
na Jeshi la Polisi upepelezi utakapokamilika atafikishwa mahakamani 
kujibu tuhuma zinazomkabili za kufanya utapeli wa kuuza madini bandia 
ambayo ni kinyume cha Sheria za nchi.
Jeshi la Polisi linatoa onyo kwa 
watu wanaojifanya wafanyabiashara wa madini kuacha mara moja tabia hiyo 
na wananchi wanaohitaji kununua madini wafike Ofisi za Wakala wa 
Madini(TMAA) ili kuepukana na matapeli.
 
 
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni