Tigo yamdhamini Ben Pol kuburudisha ‘Tamasha la Nyama Choma’
 Tamasha hilo ambalo 
linafanyika kwa mwaka wa tano sasa ni moja ya tamasha maarufu 
linalovutia watu wengi kutoka maeneo yote ya Dar es Salaam litafanyika 
kwenye viwanja vya Leaders Jumamosi Mei 28, 2016.
 Akizungumza katika mkutano na 
waandishi wa habari, Mkuu wa Tigo wa masuala ya Dijitali Paulina Shao  
alisema kuwa  kumuunga mkono Ben Pol kunaonesha  kuendelea kujikita kwa 
Tigo katika  kuwekeza katika kusaidia  sekta ya muziki ya ndani kwa 
kuhakikisha  wasanii  wanawezeshwa  kufikia viwango vya juu katika kazi 
zao.
 “Kama kampuni ya maisha ya 
kidijitali, Tigo inatambua  mchango muhimu wa wasanii wa Tanzania  
wanaoutoa katika sekta ya burudani. Hii ndio maana  tumewekeza kwa 
kiwango kikubwa  kuwasaidia wasanii  hususani wanamuziki  wa ndani 
katika kuhakikisha wanafahamika katika masoko ndani ya nchi, kikanda na 
kimataifa kwa kutumia majukwaa ya kidijitali yanayokuwepo na kushiriki  
matukio mbalimbali  na hivyo kuongeza  mauzo ya  muziki wao  pamoja na 
nembo zao,” alisema Shao.
 Aidha akiishukuru Tigo kwa 
uungwaji mkono huo, Ben Pol  aliisifu Tigo kwa juhudi  inazofanya bila 
kuchoka  katika kukuza  ukuaji wa  sekta ya muziki wa ndani  kupitia 
Jukwaa la Muziki  la Tigo.
 “Ninaishukuru sana Tigo  kwa 
uungwaji mkono ambao ni muendelezo wa mtiririko wa  programu ambazo 
imezianzisha  ili kuinua maisha ya wasanii wachanga wa Tanzania,” 
alisema Ben Pol na kutoa changamoto kwa wasanii wanaoibukia kuwa wasione
 aibu  kuomba msaada  kutoka kwa mashirika kama Tigo.
Nguli huyo wa muziki wa Bongo Flava  kwa hivi sasa anatamba na  kibao ‘MoyoMashine’ ambayo aliitoka hivi karibuni.
 Ben Pol ni miongoni mwa 
wasanii  wanaonufaika na jukwaa la Muziki la Tigo  ambalo lilianzishwa 
mwaka 2015 likiwa na lengo la  kuiunga mkono sekta ya muziki Tanzania  
kwa kuwasaidia wasanii wa ndani  kupata kipato zaidi kutokana na mauzo 
ya  kazi zao  na kuwawezesha kufahamika katika masoko ya kimataifa  
kupitia majukwaa hayo ya kidijitali  kama vile Music portal na Deezer, 
ambayo ni majukwaa ya kimataifa yaliyo kwenye mtandao yakiwa na  nyimbo 
kutoka sehemu mbalimbali  duniani  zaidi ya  milioni 36.
 
 
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni