WEMA AZINDUA MOBILE APLICATION YAKE, HABARI ZAKE ZITAPATIKANA HUMO
 Waziri
 wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Mhe. Nape Nnauye pamoja na  Miss
 Tanzania 2006 na Muigizaji maarufu wa Filamu nchini Wema Sepetu 
wakifunua pazia  kuashiria uzinduzi rasmi wa Wema Sepetu Mobile 
Application ya msanii Wema Sepetu  kwenye hoteli ya Hyyat Regency jijini
 Dar es salaam jana , Katika Aplication hiyo kutapatikana habari 
mbalimbali za msanii huyo mwigizaji wa filamu pamoja na habari 
zinazohusu masuala mbalimbali ya kazi zake hii ni kwa mara ya kwanza 
katika nchi za Afrika Mashariki kwa msanii kuwa na Mobale Aplication 
yake hivyo msanii mwingine atakayekuja atakuwa anafuata nyayo za Wema 
Sepetu.
Waziri
 wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Mhe. Nape Nnauye akihutubia 
wakati wa uzinduzi wa Wema Sepetu Mobile Application ambapo alimpongeza 
Wema kwa hatua kubwa aliyofikia ya kuwa msanii wa kwanza wa Filamu 
nchini kuwa na Mobile App na kuwataka wasanii wengine kuwa wabunifu na 
kuja na mipango ambayo itawanufaisha zaidi.
Msanii wema Sepetu akizungumza wakati wa uzinduzi wa Mobale Aplication yake kwenye hoteli ya Hyyat Regency.
Waziri
 wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Mhe. Nape Nnauye akimpongeza 
msanii  Wema Sepetuwakipiga picha ya pamoja mara baada ya uzinduzi huo.
Mtaalamu wa Mobile Application Ndugu Haji Yussuf akizungumza wakati wa uzinduzi wa Wema Sepetu Mobile Application
Waziri
 wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Mhe. Nape Nnauye akizungumza 
jambo na Miss Tanzania 2006 na Muigizaji maarufu wa Filamu nchini Wema 
Sepetu Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Mhe. Nape Nnauye 
akipiga picha ya pamoja na Miss Tanzania 2006 na Muigizaji maarufu wa 
Filamu nchini Wema Sepetu 
Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Mhe. Nape Nnauye akipiga picha ya pamoja na Miss Tanzania 2006 na Muigizaji maarufu wa Filamu nchini Wema Sepetu na mama yake kushoto pamoja Mkurugenzi wa Biashara wa kampuni ya Hartman Traders Ndugu Cecil na Mtaalamu wa Mobile Application Ndugu Haji Yussuf wa pili kutoka kushoto wakati wa uzinduzi wa mobile Application yake ambayo itawasaidia wapenzi na mashabiki wake kupata habari sahihi na za uhakika
 
 
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni