Atakeyehusisha watoto na dawa za kulevya jela miaka 30
SERIKALI imesema kuwa mtu yeyote 
atakayekamatwa kwa kosa la husisha au kushawishi mtoto kujiingiza katika
 matumizi au biashara ya dawa za kulevya atahukumiwa kifungo cha miaka 
isiyopungua 30.
Hayo yamesema na Mkuu wa Kitengo 
cha Elimu, Habari na Takwimu wa Tume ya kuratibu na kudhibiti wa Dawa za
 Kulevya, Amani Msami kupitia Taarifa ya tume hiyo kwa vyombo vya 
habari.
Msami alisema adhabu hiyo ni kwa 
mujibu wa Sheria ya kudhibiti na kupambana na Dawa za Kulevya Na.5 ya 
mwaka 2015 tofauti na Sheria ya Kuzuian Biashara Haramu ya Dawa za 
Kulevya Na. 9 ya mwaka 1995 iliyokuwa na mapungufu.
Alisema mbali na adhabu hiyo, 
sheria hiyo mpya imeweka adhabu ya kifungo cha maisha na faini ya 
shilingi Milioni 200 kwa kumiliki mitambo ya kutengeneza dawa za 
kulevya.
Msami aliongeza kuwa Sheria hiyo 
pia imeweka adhabu kali ya kifungo cha maisha pamoja na faini 
isiyopungua Shilingi Bilioni moja kwa watu wanaofadhili biashara ya Dawa
 za Kulevya.
“Aidha, sheria hii imeweka adhabu
 kali ya kifungo cha maisha pamoja na faini isiyopungua Shilingi Bilioni
 moja kwa watu wanaofadhili biashara ya Dawa za Kulevya ambao mara 
nyingi ni watu wenye uwezo,”alisema Msami.
Mkuu huyo wa Kitengo, alisema 
Serikali kupitia vyombo vya Dola iliwabaini, kuwakamata na kuwachukulia 
hatua za kisheria baadhi ya wafanyabiashara wadogo na wakubwa wa dawa za
 kulevya.
Aliwataja baadhi ya watuhumiwa 
wakubwa wa dawa hizo waliokamatwa na kuchukuliwa hatua kuwa ni  Ali 
Khatibu haji (maarufu kwa jina la Shkuba, Mohammed Mwarami (maarufu kwa 
jina la Chonji na Mwanaidi Mfundo (maarufu kwa jina la Mama Leila).
Msami alisisitiza wito wa 
Serikali kwa wananchi kutoa ushirikiano wa dhati kwa ajili ya kutoa 
taarifa kuhusu watu wanaojihusisha na biashara ya dawa ya kulevya  ili 
waweze kuchukuliwa hatua za kisheria.
 
 
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni