Naibu Spika Dkt. Tulia akabidhiwa ripoti ya uchaguzi Mkuu wa Mwaka 2015 Bungeni mjini Dodoma
Waziri
Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Kassim Majaliwa
akisalimiana na Mmbunge wa Nkasi Ali Kessy Bungeni Mjini Dodoma Mapema
leo.
Waziri
Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Kassim Majaliwa akihutubia
Bunge Mapema leo mjini Dodoma wakati wa kuhitimisha mkutano wa Tatu wa
Bunge la kumi na moja la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.
Waziri
wa Nchi Ofisi ya Rais Utumishi na Utawala Bora Mhe. Angella Kairuki
akiteta jambo na Waziri wa Elimu Sayansi na Teknolojia Mhe. Prof. Joyce
Ndalichako Bungeni Mjini Dodoma leo.
Naibu
Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Tulia
Ackson akisisitiza jambo kwa Mwenyekiti wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi
Jaji Mstaafu Damiani Lubuva na ujumbe wake uliotembelea Bunge ili
kumkabidhi Naibu Spika Ripoti ya Uchaguzi mkauu wa mwaka 2015.
Makamu
Mwenyekiti wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi Jaji Mkuu Mstaafu wa Zanzibar
Hamid Mahamud Hamid akiwa ndani ya maktaba ya Bunge wakati wa Ziara ya
Tume hiyo Bungeni Mjini Dodoma.
Naibu
Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Tulia Ackson
akiwa kwenye picha ya Pamoja na Mwenyekiti wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi
na Ujumbe wake mara baada ya ziara ya Tume hiyo Bungeni Mjini Dodoma
leo.kushoto ni Mwenyekiti wa Tume ya Mwenyekiti wa Tume ya Taifa ya
Uchaguzi Jaji Mstaafu Damian Lubuva na kulia Makamu Mwenyekiti wa Tume
ya Taifa ya Uchaguzi Jaji Mkuu Mstaafu wa Zanzibar Hamid Mahamud Hamid.
(Picha zote na Frank Mvungi-Dodoma)
———————————————————
Frank Mvungi-Dodoma
Naibu
spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania amekabidhiwa ripoti
ya uchaguzi Mkuu wa Mwaka 2015 Bungeni mjini Dodoma leo.
Akizungumza
wakati akipokea Ripoti hiyo Naibu Spika amesema kuwa ripoti hiyo ni
muhimu kwa Bunge na ni kiashiria cha ushirikiano mzuri kati ya Bunge na
Tume hiyo.
“Ushirikiano
uliopo kati ya Bunge na Tume ya Taifa ya Uchaguzi ni mzuri na kwa
upande wangu natumaini tutaendelea kushirikiana katika mambo
mbalimbali,” alisisitiza Mhe. Dkt.Tulia.
Akizungumzia
majukumu ya Bunge naibu Spika Mhe. Dkt. Tulia amesema kuwa Bunge la
kumi na moja limetimiza majukumu yake vyema hali itakayochochea
maendeleo hapa nchini katika kipindi hiki cha Serikali ya awamu ya
tano
Kwa
upande wake mwenyekiti wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi Jaji Mstaafu Damian
Lubuva amepongeza ushirikiano mzuri uliopo kati ya Tume hiyo na Bunge
kama mdau muhimu na kuahidi kuuendeleza kwa maslahi ya pande zote.
Ziara
ya Tume hiyo pamoja na kukabidhi ripoti hiyo kwa Naibu Spika ililenga
kuwajengea uwezo wajumbe wa Tume hiyo kuhusu majukumu ya Bunge ambapo
wajumbe hao walitembelea maeneo mbalimbali ya Bunge.
Tume
ya Taifa ya Uchaguzi imekabidhi ripoti ya Uchaguzi mkuu wa mwaka 2015
kwa Naibu Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt.
Tulia Ackson ikiwa ni ishara ya ushirikiano mzuri uliopo kati ya Bunge
na Tume ya Taifa ya Uchaguzi.
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni