Jumatano, 15 Juni 2016

Omar Khamis Othman amewataka wakulima wa karafuu na wadau kulilinda zao hilo

images 

MKUU wa Mkoa wa Kaskazini Pemba  Omar Khamis Othman amewataka wakulima wa karafuu pamoja na wadau wengine wa karafuu kuchukua juhudi za makusudi kulilinda  zao hilo ili liendelea kuleta tija kwa wananchi na taifa kwa ujumla .
Amesema kwamba kila mdau wa karafuu analo jukumu la kuhakikisha anaulinda mkarafuu dhidi ya vitendo vya hujuma kwa kuhakikisha zao hilo linabaki salama na mkulima ananufaika  .
 Akifunga mkutano wa wadau wa karafuu uliofanyika kwenye ukumbi za zamani wa chuo cha uwalimu benjemini mkapa Wete Mkuu hu wa  Mkoa amesema kwamba vitendo vya kukatwa mikarafuu ovyo kwa ajili ya shughuli za kijamii unapaswa kukomeshwa .
Ameeleza kuwa  kila suala la kuulinda mkrafuu dhidi ya vitendo vya hujuma si kazi ya serikali wala taasisi zake , na kuongeza hilo ni jukumu la kila mmoja bila ya kujali nafasi yake wala cheyo chake kwani  karafuu unafaida kwa jamii yote .
“Hili ni zao kuu na tegemeo la maendeleo ya uchumi wan chi , hivyo kila mmoja wetu analo jukumu la kuhakikisha kwamba anachukua hatua za kuulinda mkarafuu pamoja na karafuu dhidi ya matendo ya hujuma ”alifahamisha.
Mapema Mkurugenzi wa Mfuko wa maendeleo ya karafuu Ali Suleiman amesisitiza uwamuzi wa Shirika kutowalipa fidia watoto waliochini ya umri wa miaka 18 wanaopata ajaliw akati akichuma karafuu ..
Amesema kwa mujibu sheria za kimataifa ni kosa la jinai kumtumikisha mtoto aliye chini ya umri wa miaka 18, na uwamuzi wa Shirika pamoja na mfuko umelenga katika kumlinda mtoto dhidi ya vitendo vya utumikishwaji .
“Kwa msimu huu Shirika halitakuwa tayari kumlipa fidia mtoto aliye chini ya umri wa miaka 18,  baada ya kuanguka kwenye mkarafuu wakati akichuma karafuu , hivyo tunawaomba sana wamiliki wa mashamba ya jarafuu hakikisheni kwamba watoto hawapati nafasi ya kuchuma karafuu ”alisisitiza .
Nao baadhi ya wakulima waliliomba Shirika kuwachukulia hatua za kisheria wakulima ambao wameshindwa kurejesha mikopo , kwani wamekiuka masharti ya mikataba yao .
Walisema kuendelea kuwabembeleza wakulima hao wakati wamekiuka mikataba hiyo ni kusababisha shirika kushindwa kuwakopesha wakulima wengine kwani fedha hizo bado ziko mikononi mwa wachache .
Mkutano huo uliwashirikisha wadau wa karafuu wakiwemo wakulima , masheha , madiwani , watendaji kutoka Serikalini Kuu ambapo pia umetumika kutoa zawadi kwa wakulima bora .

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni