JESHI LA ZIMAMOTO NA UOKOAJI LAADHIMISHA WIKI YA UTUMISHI WA UMMA KWA KUTOA ELIMU YA KINGA NA TAHADHARI YA MAJANGA YA MOTO
Koplo
 wa Jeshi la Zimamoto na Uokoaji, Amani Hassan (kulia) akimuonyesha 
mwananchi aliyetembelea Banda la Maonyesho la jeshi hilo jinsi ya 
kutumia mtungi wa kuzimia moto wa awali, katika maadhimisho ya Wiki ya 
Utumishi wa Umma yanayofanyika katika viwanja vya Kituo cha Zimamoto na 
Uokoaji, Mkoa wa Ilala, jijini Dar es Salaam.
Mkaguzi
 Msaidizi wa Jeshi la Zimamoto na Uokoaji,  Idd Chanyika (kulia) akitoa 
maelezo jinsi ya vifaa vya kinga na tahadhari vinavyotumika kwa Kamishna
 wa Utawala na Fedha wa Jeshi hilo, Michael Shija (kushoto), Kamishna wa
 Oparesheni, Rogatius Kipali (wapili kushoto) na Naibu Kamishna wa 
Utawala naFedha, Billy Mwakatage walipotembelea banda hilo Kituo cha 
Zimamoto na Uokoaji, Mkoa wa Ilala, jijini Dar es Salaam.
Koplo
 wa Jeshi la Zimamoto na Uokoaji, Amani Hassan (kulia) akimuandikia 
mmoja ya mwananchi namba ya dharura 114 ambayo hutumika kupokea taarifa 
ya majanga mbalimbali kutoka kwa jamii.
Kamishna
 wa Oparesheni, Rogatius Kipali akisisitiza ufanyaji kazi kwa bidii, 
nidhamu, uadilifu na weledi kwa askari wa Jeshi la Zimamoto na Uokoaji 
wa Kituo cha Zimamoto, Mkoa wa Ilala, jijini Dar es Salaam katika 
Maadhimisho ya Wiki ya Utumishi waUumma inayofanyika katika viwanja vya 
Kituo cha Zimamoto na Uokoaji Ilala, jijini Dar es Salaam.
Banda
 la Jeshi la Zimamoto na Uokoaji lililotumika kutoa elimu ya kinga na 
tahadhari ya majanga ya moto na maokozi lililopo katika viwanja vya 
Kituo cha Zimamoto na Uokoaji, Mkoa wa Ilala, jijini Dar es Salaam. Picha zote na Godfrey Peter, Jeshi la Zimamoto na Uokoaji.
 
 
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni