ZULMIRA ATAKA KAZI KWA PAMOJA KUHAMI MAENEO YA URITHI WA DUNIA
By Newsroom on June 27, 2016
Mkuu
 wa ofisi na Mwakilishi wa Shirika la Umoja wa Mataifa linaloshughulikia
 Elimu, Sayansi na Utamaduni (UNESCO) Tanzania, Zulmira Rodrigues 
amewakumbusha wadau wa urithi wa dunia na maeneo ya hifadhi kufanyakazi 
kwa pamoja kwa lengo la kuhifadhi na kuyaendeleza maeneo hayo bila 
kuondoa ushiriki wa wananchi wanayozunguka.
Kauli
 hiyo ameitoa katika mafunzo yaliyoandaliwa na Shirika lake kwa wadau wa
 mazingira ya hifadhi na urithi wa dunia mjini Marangu Moshi, kufuatia 
makubaliano na serikali ya Tanzania.
Alisema
 akizungumza na washiriki kwamba UNESCO inachofanya ni kuanzisha safari 
ambayo inaweza kuwa ngumu na ndefu lakini washiriki wake ni lazima 
kutambua namna ya kuendelea kufanya menejimenti ya maeneo ya hifadhi na 
urithi wa dunia kwa manufaa ya kizazi cha sasa na kijacho.
Akifungua
 mafunzo hayo ambayo wataalamu ni washiriki wenyewe wakitumia njia ya 
kuelewa ya methodolojia ya uchambuzi wa vikwazo (Bottleneck Analysis 
Methodology) alisema safari ya kufanikisha menejimenti ya maeneo hayo 
duniani na hasa hapa nchini ni yenye changamoto nyingi na kwamba wadau 
wote wanatakiwa kuwa pamoja kuvishinda vikwazo hivyo na kuifanikisha 
safari.
Mkuu
 wa ofisi na Mwakilishi wa Shirika la Umoja wa Mataifa linaloshughulikia
 Elimu, Sayansi na Utamaduni (UNESCO) Tanzania, Zulmira Rodrigues 
akizungumza katika warsha ya siku tatu iliyoandaliwa na shirika lake kwa
 wadau wa mazingira ya hifadhi na urithi wa dunia iliyomalizika mwishoni
 mwa wiki mjini Marangu, mkoani Kilimanjaro.
(Picha zote na Zainul Mzige wa Modewjiblog)
 —————————————
Akizungumza
 katika warsha hiyo ambayo imechukua wadau mbalimbali wa masuala ya 
urithi na menejimenti zake kutoka serikalini, taasisi zisizo za 
kiserikali na wananchi wengine, alisema kwamba maeneo hayo yamezungukwa 
na wananchi na pamoja na kuwawekea sheria za kutoharibu na kuyachakaza 
ipo haja ya kushirikiana nao namna ya kupanga kuyaendeleza maeneo hayo 
huku yakiwa yamebaki katika hali inayotakiwa.
Mafunzo
 hayo yamelenga kuwajengea uwezo wa kupanga maendeleo katika maeneo 
ambayo ni ya urithi wa dunia, binadamu na maeneo ambayo uhai unaweza 
kuwepo.
Aidha
 akifafanua zaidi mtawala huyo wa UNESCO nchini Tanzania amesema mafunzo
 hayo yamelenga kuwapa wahusika nadharia zinazofaa katika safari ndefu 
ambayo UNESCO nayo itashiriki na isingelipenda kumwacha hata mtu mmoja 
nyuma.
Mafunzo
 hayo yanatolewa kufuatia mpango wa UNESCO wa kutaka kuwa na uhakika na 
kuhami maeneo hayo ya urithi; huku mamlaka zikitoa ushirikiano ili 
kuwezesha malengo ya maendeleo endelevu, ambayo ndiyo ajenda ya dunia 
kuelekea 2030, yanafikiwa bila kuathiri maeneo tajwa.
Ofisa
 anayeshughulikia watu na maeneo yenye uhakika wa uhai: Biashara 
zinazozingatia mazingira na uchumi unaombatana nao kutoka Sekta ya 
Sayansi Ofisi ya Unesco, Dar es salaam, Myoung Su Ko akiwasilisha mada 
kwa washiriki wa warsha hiyo iliyofanyika katika hoteli ya Kilimanjaro 
Resort mjini Marangu, mkoani Kilimanjaro.
Alisema
 kwa kuwa kitaifa, serikali imeshatoa matamko ya kisera na kuweka 
mikakati ya utekelezaji wa taratibu za kuhami maeneo ya kiutamaduni na 
ya asili ipo haja ya wadau wengine kuona namna ya kufanyakazi kama timu 
katika safari ambayo kila mmoja anastahili kuwaijibika kwa namna yake 
hata kama kunatokea changamoto.
Alisema
 wadau wanatakiwa kuangalia namna ya safari zao zinavyostahili kufanywa 
na kuwa, kwa lengo la kutumia raslimali zilizopo kutekeleza mipango ya 
maendeleo na ya kuhami maeneo hayo bila kutegemea msaada wa wafadhili au
 wahisani.
Awali
 katika ujengaji wa wazo la mafunzo ilielezwa kuwa pamoja na kuwapo na 
juhudi kubwa za kuhami maeneo ya urithi wa dunia na kuyasajili maeneo 
ambayo uhai unaweza kuwapo na wanadamu, kumekuwepo na changamoto kubwa 
za maendeleo ambazo zinatishia kuvuruga mfumo tete wa ikolojia uliopo.
Katika
 kufanikisha hifadhi ya maeneo hayo kumeonekana changamoto za upungufu 
wa rasilimali watu wenye uwezo na vifaa vya kushughulikia uharibifu, 
ukosefu wa uwezo wa kuhifadhi maeneo hayo kwa kuoanisha na uwapo wa 
watu.
Mtaalamu
 wa programu na utamaduni kutoka Ofisi za Unesco Afrika Mashariki Bi. 
Karalyn Monteil akiwasilisha mada kuhusu makubaliano ya ulinzi katika 
maeneo ya urithi na utamaduni wa dunia katika warsha hiyo iliyomalizika 
mwishoni mwa juma mjini Marangu, Moshi.
 
 
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni