Mh. Herman Kapufi aipongeza Mamlaka ya Elimu Tanzania (TEA) katika kuendeleza sekta ya elimu nchini.
Na Hassan Silayo
Aliyekuwa Mkuu wa Wilaya ya Same 
Mh. Herman Kapufi ameshukuru Jitihada zinazofanywa na Mamlaka ya Elimu 
Tanzania (TEA) katika kutekeleza miradi inayosaidia kuongeza ubora wa 
elimu nchini ikiwemo utekelezaji wa mradi kukarabati shule kongwe nchini
 utakaoboresha mazingira ya kufundishia na kusaidia kuinua kiwango cha 
elimu katika shule hizo.
Mh. Kapufi amesema kuwa mpango 
huo umekuja wakati muafaka wakati uongozi wa wilaya hiyo ukipambana 
kutatua changamoto za elimu na kuwataka wadau kuipa ushirikiano Mamlaka 
hiyo.
“Kwa kweli napenda kuishukuru 
Mamlaka ya elimu Tanzania kwa jitihada zake hizi za kuboresha sekta ya 
elimu nchini, kwa kweli wamefanya kazi kubwa sana katika wilaya hii kwa 
kipindi chote nilichokuwa hapa kama mkuu wa wilaya, shule zetu kongwe 
zimechoka sana na zinahitaji ukarabati ili kuweza kuzirudisha katika 
hali yake ya kawaida kwa utekelezaji wa mpango huu” Alisema Mh.Kapufi.
Naye Meneja Mawasiliano na 
Uhusiano wa Mamlaka ya Elimu Tanzania Bibi. Sylvia Lupembe amesema kuwa 
kupitia TEA mpango huo utatekelezwa katika shule kongwe 11 katika mikoa 
ya Bukoba, Mwanza, Tabora, Singida, Same, Arusha, Dodoma, Morogoro na 
Pwani kwa kuzifanyia ukarabati wa miundo mbinu mbalimbali ikiwemo 
madarasa, vyoo, maabara, mabweni na mifumo ya umeme.
“hali ya shule zetu kongwe kwa 
kweli sio nzuri tumetembea kwenye mikoa takribani Mikoa sita tumejionea 
halihalisi ya miundombinu ya shule zetu kongwe hazipo katika mazingira 
mazuri ya kujifunzia kutokana na kuwa na miundombinu chakavu na kwa 
mradi huu tunataka kuweka mazingira mazuri ya watoto wetu hawa 
kujifunzia hasa kwa kuanza na shule hizi kongwe” Alisema Sylvia.
Wakizungumzia ukarabati huo 
Mwalimu Mkuu wa shule wa Shule ya Sekondari Nganza Bi. Yacinta Lyimo 
aliishukuru Mamlaka ya Elimu Tanzania (TEA) kwa Utekelezaji wa mpango 
huo kwani utasaidia kuboresha mazingira ya kufundishia na hata kusaidia 
kuinua kiwango cha elimu  na ufaulu katika shule hizo.
Aidha, Afisa Elimu wa Manispaa ya
 Singida Bw. Omari Kisuda Mpango huu wa maboresho ya shule kongwe ni 
mkombozi katika sekta ya elimu na umekuja wakati uhitaji wa maboresho ya
 shule hizo unahitajika hasa kutokana na baadhi ya shule kushindwa 
kufanya ukarabati wa mara kwa mara kutokana na ufinyu wa bajeti.
 
 
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni