MATUKIO KATIKA PICHA BUNGENI DODOMA
Waziri
 wa Viwanda Biashara na Uwekezaji Mhe. Charles Mwijage akijibu maswali 
ya Wabunge Leo Bungeni Mjini Dodoma kuhusu mpango wa Serikali wa 
kuimarisha Viwanda  vilivyopo hapa nchini na kujenga vipya katika Mikoa 
mbalimbali.
Waziri
 wa Elimu Sayansi Teknolojia na Mafunzo ya ufundi Mhe. Dkt. Joyce 
Ndalichako akieleza juu ya mkakati wa Serikali kuimarisha vyuo vya 
Ufundi Stadi hapa nchini wakati wa kipindi cha maswali na majibu Bungeni
 Mjini Dodoma.
Waziri
 wa Katiba na Sheria Mhe. Dkt. Harrison Mwakiyembe akiteta jambo na 
Mbunge wa Korogwe Vijijini Mhe. Steven Ngonyani Bungeni Mjini Dodoma 
Leo.
Waziri
 wa Fedha na Mipango Dkt.Philip Mpango  akijibu hoja za wabunge kuhusu 
Muswada wa Marekebisha ya Sheria ya Ununuzi wa Umma wa mwaka 2016 Leo 
Bungeni Mjini Dodoma.
Naibu
 Waziri Wizara ya Ujenzi Uchukuzi na Mawasiliano Mhe. Edwin Ngonyani 
akitoa ufafanuzi kuhusu mikakati ya Serikali kuimarisha miundombinu ya 
Barabara hapa Nchini.
Naibu
 Waziri Wizara ya Ujenzi Uchukuzi na Mawasiliano Mhe. Edwin Ngonyani 
akitoa ufafanuzi kuhusu mikakati ya Serikali kuimarisha miundombinu ya 
Barabara hapa Nchini.
Mbunge
 Viti Maalum Mhe. Martha Mlata akichangia hoja wakati wa uwasilishwaji 
wa Muswada wa Marekebisho ya Sheria ya Ununuzi wa Umma wa mwaka 2016.
Baadhi ya Wabunge wakimpongeza Waziri wa Fedha na Mipango Mhe. Dkt. 
Philip Mpango (wa katikati) mara baada ya kupitishwa kwa muswada wa 
Marekebisho ya Sheria ya Ununuzi wa Umma.
(Picha zote na Frank Mvungi-Dodoma)
 
 
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni