Zaidi ya wilaya 81 kuongezewa usikivu wa redio ya Taifa
————————–
Zaidi
 ya Wilaya 81 ambazo zimekuwa hazipati usikivu wa redio ya Taifa nchini 
kuongezewa usikivu kwa mwaka wa fedha 2016/17 na kuendelea.
Hayo 
yamesemwa na Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Mhe. Nape 
Nnauye leo Mjini Dodoma alipokuwa akijibu swali la Mbunge wa Nachingwea 
Mhe. Hasani Eliasi Masala juu ya kutokusikika redio ya Taifa katika 
jimbo lake.
Aidha
 Mhe. Nape amesema kuwa kutosikika kwa redio ya Taifa katika Wilaya hiyo
 kumetokana na uchakavu wa mitambo, lakini kwa hivi sasa eneo la 
Nachingwea Mjini linapata matangazo ya redio ya Taifa kwa kutumia 
mitambo miwili midogo ya Redio-FM ya TBC-FM na mtambo wa TBC-Taifa.
“Nia 
ya Serikali ni kufunga mitambo mipya na ya kisasa ya FM yenye nguvu 
kubwa ya kilowati 2 ambao utakuwa na uwezo wa kurusha matangazo 
yatakayowafikia wananchi sehemu mbali mbali nchi nzima,” alifafanua Mhe.
 Nape.
Aliendelea
 kwa kusema kuwa, tathmini iliyofanyika kubaini usikivu wa redio ya 
Taifa nchini umeonyesha kuwa jumla ya wilaya 81 hazina usikivu mzuri wa 
redio ya Taifa kutokana na uchakavu wa mitambo. 
Aidha
 Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo imejipanga kufunga 
mitambo mipya, sambamba na ukarabati wa majengo ya mitambo, ofisi na 
miundo mbinu mbalimbali kuanzia mwaka wa fedha 2016/2017 na kuendelea 
kwa kuanza na Mikoa iliyopo pembezoni ili kuboresha usikivu ikiwezekana 
isikike mpaka nchi jirani.
 
 
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni