Maombi Maalumu Kwa Ajili ya Kumuombea Rais Magufuli na Tanzania Katika Kanisa la IEAGT Shinyanga
Hapa
ni ndani ya kanisa la The International Evangelical Assemblies Of God
–Tanzania (IEAGT) lililopo katika kata ya Kambarage katika manispaa ya
Shinyanga ambapo leo Jumapili Juni 26,2016 kumefanyika Maombi Maalumu
kwa ajili ya taifa la Tanzania, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
Dkt John Pombe Magufuli,makamu wa rais,bunge,mahakama,polisi na viongozi
mbalimbali wa serikali.
—————————————————–
Maombi
hayo yameongozwa na askofu wa kanisla la (IEAGT) David Elias Mabushi na
kuhudhuriwa na kaimu mkuu wa mkoa wa Shinyanga Mheshimiwa Josephine
Matiro ambaye ni mkuu wa wilaya ya Shinyanga.
Maombi
hayo pia yamehudhuriwa na viongozi mbalimbali wa serikali,vyama vya
siasa,mashirika,waandishi wa habari,wageni mbalimbali na waumini wa
kanisa hilo.
Pamoja
na maombi hayo maalumu, Kanisa hilo limeadhimisha siku ya watoto
katika kanisa hilo ambapo pia Juni 26 ni siku ya kuzaliwa kwa askofu wa
kanisa la IEAGT David Mabushi ambaye leo ametimiza umri wa miaka 53.
Sambamba
na matukio hayo mawili makubwa,kanisa hilo pia lilikabidhi madawati 20
kwa uongozi wa wilaya ya Shinyanga kwa ajili ya kumuunga mkono rais
Magufuli katika jitihada zake za kuhakikisha kuwa changamoto ya madawati
inamalizika katika shule.
Awali
akisoma risala,Katibu wa kanisa la IEAGT, Mchungaji Obed Jilala alisema
baada ya uchaguzi mkuu 2015,kanisa la IEAGT limekuwa likisikia kwa
nyakati tofauti rais Magufuli akiomba maombi kwa ajili ya kazi yake ya
kuliongoza taifa,hivyo kanisa lao limeguswa sana na kauli hiyo na katika
kuonesha wanamuunga mkono walikubaliana siku ya Jumapili Juni 26,2016
iwe ya maombi maalumu kwa ajili ya kiongozi wa taifa sambamba na
kuliombea nchi ya Tanzania.
“Maombi
haya yamebebwa kwa kiasi kikubwa na upendo tulio nao kwa nchi yetu
,kanisa la IEAGT kama sehemu ya jamii ya watanzania tumeona siku ya leo
iwe kilele cha maombi ya kitaifa katika mkoa wetu na mahali popote
lilipo kanisa letu”,aliongeza Mchungaji Jilala.
Naye
Askofu wa kanisa hilo David Mabushi akitoa mahubiri yake,mbali na
kumpongeza rais Magufuli kwa kuchaguliwa kuwa rais,alimuomba kuendelea
kuonesha msimamo wake katika kuwaletea maendeleo watanzania huku
akimfananisha na Nabii Musa akisema Magufuli amekuja kuiokomboa nchi na
kuifanya kuwa nchi ya asali na maziwa.
“Tumeandaa
siku hii muhimu kwa ajili ya kuiombea nchi yetu ili iendelee kuwa na
amani,tunamuombea rais wetu kwa sababu wenye haki wakiwa na amri,watu
hufurahi..sisi kama kanisa tutahakikisha tunamuunga mkono rais Magufuli
kwa maneno na vitendo ndiyo maana leo tunatoa sadaka ya madawati
20,tunaomba watanzani waendelee kumuombea rais wetu aliyeonesha kuwajali
watanzania tangu alipoingia madarakani amekuwa mstari wa mbele kupigana
dhidi ya rushwa na vitendo vyote viovu”,aliongeza askofu Mabushi.
Kwa
upande wake mgeni rasmi Kaimu Mkuu wa mkoa wa Shinyanga ,Josephine
Matiro ambaye ni Mkuu wa wilaya ya Shinyanga Josephine
Matiro,alilipongeza kanisa hilo kuona umuhimu wa kuombea viongozi wa
nchi na kuongeza kuwa kanisa la IEAGT ni kanisa la kwanza mkoani
Shinyanga kufanya maombi kwa ajili ya viongozi wa nchi.
“Ndugu
zangu watanzania naomba tuendelee kuiombea nchi ili iendelee kuwa ya
amani na viongozi kuwa na hofu ya mungu,lakini pia naomba watanzania
wafanye kazi,sasa ni muda wa kuchapa kazi tuache siasa za
majukwaani,tumuunge mkono mheshimiwa rais katika kutekeleza kauli mbiu
ya Hapa Kazi tu”,aliongeza Matiro
Continue reading →
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni