Maombi Maalumu Kwa Ajili ya Kumuombea Rais Magufuli na Tanzania Katika Kanisa la IEAGT Shinyanga
Hapa
 ni ndani ya kanisa la The International Evangelical Assemblies Of God 
–Tanzania (IEAGT) lililopo katika kata ya Kambarage katika manispaa ya 
Shinyanga ambapo leo Jumapili Juni 26,2016 kumefanyika Maombi Maalumu 
kwa ajili ya taifa la Tanzania, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania 
Dkt John Pombe Magufuli,makamu wa rais,bunge,mahakama,polisi na viongozi
 mbalimbali wa serikali.
 —————————————————–
Maombi
 hayo yameongozwa na askofu wa kanisla la (IEAGT) David Elias Mabushi na
 kuhudhuriwa na kaimu mkuu wa mkoa wa Shinyanga Mheshimiwa Josephine 
Matiro ambaye ni mkuu wa wilaya ya Shinyanga.
Maombi
 hayo pia yamehudhuriwa na viongozi mbalimbali wa serikali,vyama vya 
siasa,mashirika,waandishi wa habari,wageni mbalimbali na waumini wa 
kanisa hilo.
Pamoja
 na maombi hayo maalumu, Kanisa hilo  limeadhimisha siku ya watoto 
katika kanisa hilo ambapo pia Juni 26 ni siku ya kuzaliwa kwa askofu wa 
kanisa la IEAGT David Mabushi ambaye leo ametimiza umri wa miaka 53.
Sambamba
 na matukio hayo mawili makubwa,kanisa hilo pia lilikabidhi madawati 20 
kwa uongozi wa wilaya ya Shinyanga kwa ajili ya kumuunga mkono rais 
Magufuli katika jitihada zake za kuhakikisha kuwa changamoto ya madawati
 inamalizika katika shule.
Awali
 akisoma risala,Katibu wa kanisa la IEAGT, Mchungaji Obed Jilala alisema
 baada ya uchaguzi mkuu 2015,kanisa la IEAGT limekuwa likisikia kwa 
nyakati tofauti rais Magufuli akiomba maombi kwa ajili ya kazi yake ya 
kuliongoza taifa,hivyo kanisa lao limeguswa sana na kauli hiyo na katika
 kuonesha wanamuunga mkono walikubaliana siku ya Jumapili Juni 26,2016 
iwe ya maombi maalumu kwa ajili ya kiongozi wa taifa sambamba na 
kuliombea nchi ya Tanzania.
“Maombi
 haya yamebebwa kwa kiasi kikubwa na upendo tulio nao kwa nchi yetu 
,kanisa la IEAGT kama sehemu ya jamii ya watanzania tumeona siku ya leo 
iwe kilele cha maombi ya kitaifa katika mkoa wetu na mahali popote 
lilipo kanisa letu”,aliongeza Mchungaji Jilala.
Naye
 Askofu wa kanisa hilo David Mabushi akitoa mahubiri yake,mbali na 
kumpongeza rais Magufuli kwa kuchaguliwa kuwa rais,alimuomba kuendelea 
kuonesha msimamo wake katika kuwaletea maendeleo watanzania huku 
akimfananisha na Nabii Musa akisema Magufuli amekuja kuiokomboa nchi na 
kuifanya kuwa nchi ya asali na maziwa.
“Tumeandaa
 siku hii muhimu kwa ajili ya kuiombea nchi yetu ili iendelee kuwa na 
amani,tunamuombea rais wetu kwa sababu wenye haki wakiwa na amri,watu 
hufurahi..sisi kama kanisa tutahakikisha tunamuunga mkono rais Magufuli 
kwa maneno na vitendo ndiyo maana leo tunatoa sadaka ya madawati 
20,tunaomba watanzani waendelee kumuombea rais wetu aliyeonesha kuwajali
 watanzania tangu alipoingia madarakani amekuwa mstari wa mbele kupigana
 dhidi ya rushwa na vitendo vyote viovu”,aliongeza askofu Mabushi.
Kwa
 upande wake mgeni rasmi Kaimu Mkuu wa mkoa wa Shinyanga ,Josephine 
Matiro ambaye ni Mkuu wa wilaya ya Shinyanga Josephine 
Matiro,alilipongeza kanisa hilo kuona umuhimu wa kuombea viongozi wa 
nchi na kuongeza kuwa kanisa la IEAGT ni kanisa la kwanza mkoani 
Shinyanga kufanya maombi kwa ajili ya viongozi wa nchi.
“Ndugu
 zangu watanzania naomba tuendelee kuiombea nchi ili iendelee kuwa ya 
amani na viongozi kuwa na hofu ya mungu,lakini pia naomba watanzania 
wafanye kazi,sasa ni muda wa kuchapa kazi tuache siasa za 
majukwaani,tumuunge mkono mheshimiwa rais katika kutekeleza kauli mbiu 
ya Hapa Kazi tu”,aliongeza Matiro
 Continue reading →
 
 
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni