WAFANYAKAZI WA ABANA WAANDAMANA KUDAI MIL 400 WANAZODAI
(Picha na Mwamvua Mwinyi) 
———————————————————–
———————————————————–
Na Mwamvua Mwinyi,Bagamoyo
WAFANYAKAZI
 wa kiwanda cha uchapishaji vitabu(ABANA Printers Ltd) kilichopo kata ya
 Mapinga wilayani Bagamoyo mkoani Pwani ,wanadai fedha za mishahara na 
mafao yao kiasi cha sh.mil.400 tangu mwaka 2014 bila mafanikio.
Aidha
 wafanyakazi hao waiomba serikali ya awamu ya tano kuingilia kati tatizo
 hilo kwani wameshapigania haki zao kupitia mahakamani ,wizara,idara na 
vyama vinavyojishughulisha kutetea haki za wafanyakazi lakini hakuna 
msaada walioupata.
Wameeleza
 kuwa hadi sasa wanaishi katika maisha magumu  huku wengine wakiwa 
wamefukuzwa kwenye nyumba walizopanga  na wenzao watatu wamefariki 
kutokana na ugonjwa wa moyo.
Hayo 
yamejiri jana baada ya wafanyakazi hao kuchukua hatua ya kufanya 
maandamano nje ya kiwanda hicho na kisha kumfikishia kilio chao 
mwenyekiti wa jumuiya ya wazazi (CCM)Bagamoyo,alhaj Abdul Sharif ili 
aweze kuwasaidia kulipwa haki zao.
Mwenyekiti
 wa tawi la chama cha wafanyakazi tawi la ABANA printers Wilbard Ikigo 
,alidai kuwa mmiliki wa kampuni hiyo anajigamba kwa kusema serikali ipo 
mkononi mwake hivyo hawezi kuchukuliwa hatua yoyote.
Alisema
 ni miaka miwili na nusu sasa tangu watelekezwe na mwajiri wao hali 
iliyosababisha kuingia katika mgogoro na mmiliki huyo.
 
 
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni