Mkurugenzi
Mkuu wa Ofisi ya Taifa ya Takwimu Dkt. Albina Chuwa akizungumza leo
jijini Dar es Salaam katika hafla ya kukabidhiana magari tisa yenye
thamani ya Shillingi Millioni mia nane na kumi kutoka Shirika la ICAP
Tanzania kwa ajili ya Utafiti wa Viashiria na Matokeo ya UKIMWI Tanzania
utakaofanyika nchi nzima kuanzia mwezi Septemba, 2016. Kushoto kwake ni
Claud Kumalija mwakilishi wa katibu Mkuu wa Wizara Afya, Maendeleo ya
Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto.
Mwenyekiti
wa Tume ya Kudhibiti UKIMWI (TACAIDS), Dkt. Fatuma Mrisho akizungumza
leo jijini Dar es Salaam katika hafla ya kukabidhiana magari tisa yenye
thamani ya Shillingi Millioni mia nane na kumi kati ya Ofisi ya Taifa ya
Takwimu na Shirika la ICAP Tanzania kwa ajili ya Utafiti wa Viashiria
na Matokeo ya UKIMWI Tanzania utakaofanyika nchi nzima kuanzia mwezi
Septemba, 2016. Kushoto kwake ni Claud Kumalija mwakilishi wa katibu
Mkuu wa Wizara Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto na
kulia kwake ni Dkt. Michelle Roland Mkurugenzi Mkaazi wa Taasisi ya
Marekani ya Kudhibiti Magonjwa – (Centre for Disease Control and
Prevention – CDC).
Mkurugenzi
Mkaazi wa Shirika wa Taasisi ya Marekani ya Kudhibiti Magonjwa –
(Centre for Disease Control and Prevention – CDC) Dkt. Michelle Roland
akikata utepe kuashiria kukabidhi rasmi magari tisa yenye thamani ya
Shillingi Millioni mia nane na kumi kwa Ofisi ya Taifa ya Takwimu kwa
ajili ya Utafiti wa Viashiria na Matokeo ya UKIMWI Tanzania
utakaofanyika nchi nzima kuanzia mwezi Septemba, 2016.
Mkurugenzi
Mkuu wa Ofisi ya Taifa ya Takwimu Dkt. Albina Chuwa pamoja na
mwakilishi wa katibu Mkuu wa Wizara Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia,
Wazee na Watoto Claud Kumalija wakionyesha ufunguo wa gari mbele ya
waandishi wa habari na wageni waalikwa kuashiria kupokea magari tisa
yaliyotolewa na Shirika la ICAP Tanzania kwa ajili ya Utafiti wa
Viashiria na Matokeo ya UKIMWI Tanzania utakaofanyika nchi nzima kuanzia
mwezi Septemba, 2016.
Mkurugenzi
Mkuu wa Ofisi ya Taifa ya Takwimu Dkt. Albina Chuwa akiwasha gari kama
ishara ya kupokea magari tisa yenye thamani ya Shillingi Millioni mia
nane na kumi kutoka Shirika la ICAP Tanzania kwa ajili ya Utafiti wa
Viashiria na Matokeo ya UKIMWI Tanzania utakaofanyika nchi nzima kuanzia
mwezi Septemba, 2016. Hafla ya makabidhiano ya magari hayo imefanyika
leo jijini Dar es Salaam.
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni