Rais Magufuli Awataka wakuu wa Wilaya na mikoa kuchapa kazi.
Na Daudi Manongi,MAELEZO
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa 
Tanzania Mhe.Dkt John Pombe Magufuli amewataka wakuu wa wilaya na mikoa 
kuchapa kazi kwa bidii kwani viongozi hao ndio wawakilishi wa wananchi 
wa vijijini.
Mhe.Rais Magufuli ameyasema hayo 
alipokuwa akizungumza wakati wakuu wa wilaya na mikoa walipokuwa Ikulu 
wakila kiapo cha maadili ya viongozi kabla ya kwenda kuapishwa na wakuu 
wa mikoa yao.
Rais Magufuli pia amewataka 
viongozi hao kufanya kazi na kutimiza majukumu yao kwani wananchi wana 
changamoto nyingi,na wao waende kutatua matatizo ya wananchi walio 
maskini.
Aidha amewataka viongozi hao 
kutokuwa chanzo cha kutengeneza matatizo katika jamii na hivyo wasimamie
 haki na ukweli,wasiwe wala rushwa,wazingatie maadili na kuwatumikia 
wananchi wote bila kujali itikadi za vyama zao,dini au kabila uku 
akiwataka kutekeleza waliyohaidi kwenye ilani ya chama cha mapinduzi.
Pia amewataka viongozi hao kuweke
 mkazo katika kutatua kero za wananchi na kuwataka kutimiza kwa vitendo 
kwa kushirikiana na viongozi watakaowakuta katika maeneo yao 
waliyopangiwa.
Hata hivyo amewataka viongozi hao
 kusimamia mapato ya Serikali katika miradi yote kwenye maeneo yao ili 
kuhakikisha serikali inapata kodi ambayo itasaidia katika maendeleo ya 
Taifa hili.
 
 
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni