MWINYIMVUA: Awataka Watumishi kuzingatia maadili ya Utumishi wa Umma
Katibu
 Mkuu Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera na Uratibu) Dkt. Hamisi Mwinyimvua 
akisoma maelekezo kuhusu umuhimu wa kuzingatia maadili ya Utumishi wa 
Umma kwa wafanyakazi wa Ofisi yake jijini Dar es Salaam tarehe 22 Juni, 
2016 (hawapo pichani) wakati wa maadhimishi ya Wiki ya Utumishi wa Umma 
yanayoadhimishi kila mwaka Barani Afrika Juni 16-23.
Baadhi
 ya Watumishi wa Ofisi ya Waziri Mkuu wakimsikiliza Katibu Mkuu Ofisi ya
 Waziri Mkuu (Sera na Uratibu) Dkt. Hamisi Mwinyimvua wakati wa 
maadhimisho ya Wiki ya Utumishi wa Umma yaliyoadhimishwa ofisi hapo.
Baadhi
 ya Watumishi wa Ofisi ya Waziri Mkuu wa Idara ya Mpigachapa Mkuu wa 
Serikali wakimsikiliza Katibu Mkuu Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera na 
Uratibu) Dkt. Hamisi Mwinyimvua (hayupo pichani) wakati wa maadhimisho 
ya Wiki ya Utumishi wa Umma yaliyoadhimishwa ofisi hapo.
(PICHA ZOTE NA OFISI YA WAZIRI MKUU)
……………………………………………………………………………………………..
Na. wandishi Wetu
Katibu Mkuu Ofisi ya Waziri Mkuu 
(Sera na Uratibu) Dkt. Hamisi Mwinyimvua amewataka Wafanyakazi Ofisi ya 
Waziri Mkuu kuzingatia maadili na kanuni za Utumishi wa Umma wakati wa 
Maadhimisho ya wiki ya Utumishi wa Umma.
Dkt. Mwinyimvua amesema hayo 
tarehe 22 Juni, 2016 Ofisini kwake Jiji Dar es salaam,  wakati ofisi 
yake ikiadhimisha wiki ya Utumishi wa Umma ambayo kila mwaka 
huadhimishwa Juni 16 – 23, 2016 Barani Afrika ambapo kauli mbiu ya mwaka huu ni “Uongozi wa Umma kwa Ukuaji Jumuishi: Kuelekea katika Afrika tunayoitaka”.
“Kila mtumishi wa umma anapaswa 
kuzingatia maadili na sheria za utumishi wa umma ambazo ndio nguzo ya 
kuimarisha utendaji kazi na kuimarisha misingi na maadili ya Umma” 
alisema Dkt. Mwinyimvua”. 
Kuna sheria ya Utumishi wa Umma 
ya mwaka 2002, maboresho ya Kanuni ya Utumishi wa Umma ya mwaka 2009 na 
miongozo mbalimbali inayoelekeza namna na jinsi mtumishi wa umma 
anapaswa kuifuata.
“Nafahamu zipo changamoto nyingi 
ambazo zinawapata watumishi wa umma nataka niwahakikishie kwamba, 
serikali inazitambua na inazifanyia kazi hivyo nawasii tufanye kazi kwa 
bidii kwani tunatambua kauli mbiu ya Serikali ya Mhe. Rais John Pombe 
Magufuli ya Hapa Kazi tu inabidi kuitekeleza kwa kufanya kazi na tuache kufanya kazi kwa mazoea”, alisisitiza Dkt. Mwinyimvua.
Tumie mda wenu kujisomea vitabu, 
Magazeti, Vijarida, vitawasaidia kujifunza na kupata maarifa tofauti 
ambayo yataweza kuwasaidia kuwa wabunifu katika sehemu zenu za kazi, 
elimu na maarifa inapatikana kwa kujisomea tujijengee mazingira hayo 
yatawasaidia kuwaongezea ufanisi wa kazi, alisema Dkt. Mwinyimvua. 
Kwa mwaka huu maadhimisho ya Wiki
 ya Utumishi wa Umma yanaadhimishwa na Wizara na Taasisi za Serikali kwa
 kukutana na watumishi wa umma na wadau mbalimbali kwa lengo la kupokea 
changamoto, maoni, ushauri ikiwa ni lengo la Serikali la kutaka 
kuboresha huduma kwa wananchi.  
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni