Jumatano, 29 Juni 2016

MBUNGE TUNDU LISSU AWEKWA LUMANDE BAADA YA KUKOSA DHAMANA


Na Mwandishi wetu, Dar
MBUNGE wa Jimbo la Singida Mashariki (Chadema),Tundu Lissu amewekwa lumande baada ya kukosa dhamana.

Kukosa dhamana hiyo kunafuatia kwa Mbunge Lissu kuripoti katika kituo cha polisi kanda maalumu ya Dar es Salaam leo hii kwa ajili ya kuhojiwa na jeshi hilo kuhusu kauli aliyoitoa jana baada ya kutoka Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu jijini Dar es Salaam.

Mbunge huyo amehojiwa kwa saa tatu kuhusiana na maneno mengine ambayo ameyaandika kupitia mitandao ya kijamii yanayodaiwa kuwa ni ya uchochezi.


Akizungumza na waandishi wa habari katika kituo cha polisi kanda maalumu ya Dar es Salaam leo,Mbunge wa Arusha mjini,Godbles Lema amekili kuwa Lissu amewekwa lumande kwa kukosa dhamana na hataachiwa leo atalala lumande.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni