SMZ YAAHIDI KUENDELEZA MIPANGO YA UCHUMI INAYOCHAGIZWA KIMATAIFA
SERIKALI
 ya Mapinduzi ya Zanzibar imesema itaendelea kuhakikisha mipango yote ya
 kimaendeleo inayochagizwa na malengo endelevu ya kimataifa inatekelezwa
 kwa vitendo ili wananchi waweze kunufaika.
Imesema
 katika malengo ya milennia ya 2015 serikali ilifanikiwa katika baadhi 
ya sekta zikiwemo sekta za elimu, afya na miundo mbinu hatua 
zinazotakiwa kuendelea kupewa kipaumbele na wadau wa maendeleo.
Kauli
 hiyo imetolewa na Katibu Mtendaji wa Tume ya Mipango Zanzibar, Juma 
Reli katika Mkutano wa wadau wa sekta za maendeleo nchini wanaojadili 
utekelezaji wa Malengo ya Maendeleo Endelevu (SDG’s) visiwani humo. 
Mkutano huo ulifanyika katika Hoteli ya Zanzibar Ocean View.
Alisema
 licha ya kuwepo na changamoto mbali mbali za kiutendaji katika 
utekelezaji wa mipango hiyo ikiwemo suala la wananchi kutokuwa na uelewa
 mzuri wa Malengo ya Maendeleo Endelevu ya dunia bado mamlaka husika 
zinaendelea kutoa elimu hiyo.
Mkurugenzi
 Mtendaji wa Taasisi ya Utafiti wa Uchumi na Kijamii (ESRF), Dkt. Tausi 
Kida akitoa neno la ukaribisho katika Mkutano wa wadau wa sekta za 
maendeleo nchini wanaojadili utekelezaji wa Malengo ya Maendeleo 
Endelevu (SDG’s) visiwani Zanzibar ambao umeandaliwa na ESRF kwa 
kushirikiana na Tume ya Mipango Zanzibar chini ya ufadhili wa Shirika la
 Maendeleo la Umoja wa Mataifa (UNDP) nchini.
Reli
 alieleza kwamba malengo na mipango mbalimbali ya maendeleo ni 
kuwasaidia wananchi wa Zanzibar waweze kuondokana na tatizo sugu la 
umaskini, magonjwa na changamoto za kiusalama.
“Katika
 MDG tumeweza kufanikiwa kwa baadhi ya malengo ikiwemo suala la elimu na
 afya lakini kuna mengine bado hatukuweza kufanikiwa kuyafikia na kwa 
sasa tunaendelea na malengo mapya ya SDG’s ambayo tunatakiwa kuyafanyia 
kazi ili yaende sambamba na mipango ya Serikali ya Mapinduzi ya 
Zanzibar.” alisema Reli.
Aidha
 alisema bado wanajadiliana ni kwa namna gani mipango ya kimataifa 
tutaiingiza katika sera na mipango yetu ya kimaendeleo ili wananchi 
waweze kunufaika na fursa hizo za kimaendeleo na kiuchumi kwa ufanisi 
zaidi.
Alisema
 utekelezaji wa Malengo ya Maendeleo Endelevu SDG’s ambayo ni 17 
yanatakiwa kupewa kipaumbele kwani yanagusa nyanja mbalimbali za kijamii
 yakiwemo maisha halisi ya wananchi wanaostahiki kunufaika na fursa na 
mahitaji muhimu ya kibinadamu.
Mwakilishi
 wa Umoja wa Mataifa (UN) Ofisi ya Zanzibar, Anna Senga akizungumza kwa 
niaba ya Mkuu wa Mashirika ya Umoja wa Mataifa nchini, Bw. Alvaro 
Rodriguez katika mkutano wa wadau wa sekta za maendeleo nchini kujadili 
utekelezaji wa Malengo ya Maendeleo Endelevu (SDG’s) visiwani Zanzibar.
Kwa
 Upande wake, Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Utafti, Uchumi na 
Kijamii nchini ( ESRF), Dkt.Tausi Kida akitoa neno la ukaribisho 
alisema, ili kufikia malengo yaliyokusudiwa katika SDG’s ni vyema sera 
na mipango endelevu ya nchi husika iweke vipaumbele vya kukuza uchumi 
kuanzia ngazi za chini
Kida
 alieleza kwamba katika utekelezaji wa SDG’s lazima kuwepo na mpango 
endelevu wa ufuatiliaji kuanzia ngazi za chini hadi taifa kwa lengo la 
kuhakikisha malengo hayo yanatekelezwa kwa mujibu wa matakwa ya malengo 
ya kimataifa.
Naye
 Mwakilishi wa Umoja wa Mataifa (UN), Ofisi ya Zanzibar, Anna Senga 
alisema endapo malengo ya dunia yataweza kutekelezwa ipasavyo Zanzibar 
itaweza kupunguza changamoto mbali mbali zinazokabili sekta za kijamii 
na kiuchumi.
Alisema
 UN itaendelea kuunga mkono juhudi zinazofanywa na Serikali ya Mapinduzi
 Zanzibar katika utekelezaji wa SDG’s kama ilivyokuwa katika utekelezaji
 wa malengo ya dunia MDG’s yaliyopita ili serikali iweze kufikia ngazi 
za chini kwa kuinua kipato cha wananchi kiendane na ukuaji wa uchumi wa 
nchi.
Mgeni
 rasmi Katibu Mtendaji wa Tume ya Mipango Zanzibar, Juma Reli akitoa 
nasha wakati akifungua mkutano wa siku moja wa wadau wa sekta za 
maendeleo nchini wa kujadili utekelezaji wa Malengo ya Maendeleo 
Endelevu (SDG’s) visiwani Zanzibar ambao umefanyika katika Hoteli ya 
Zanzibar Ocean View.
Senga
 aliishauri serikali ya Mapinduzi Zanzibar kuendelea kuwashirikisha 
wananchi wa ngazi za chini katika kupanga na kutekeleza maendeleo yao 
katika maeneo husika ya wananchi.
“Changamoto
 zinazojitokeza katika utekelezaji wa malengo ya maendeleo ya kimataifa 
ili yaendane na mipango ya maendeleo ya serikali ni upungufu wa 
ushirikishwaji wa wananchi ama jamii husika na wengine hawafikiwi kabisa
 katika maeneo yao jambo linalotakiwa kufanyiwa kazi kwa haraka katika 
kutekeleza kwa vitendo Malengo ya Maendeleo Endelevu ya SDG’s”, 
alifafanua Senga.
Naye
 Mshauri wa Masuala ya Uchumi wa Shirika la Umoja wa Mataifa la 
Maendeleo (UNDP) Tanzania, Rogers Dhliwayo alisema Malengo ya Maendeleo 
Endelevu SDG’s yanatakiwa yawekewe vipaumbele mbalimbali vya takwimu na 
tafti za kiuchumi katika maeneo tofauti ya jamii ili malengo endelevu 
yaweze kuwafikia walengwa.
Kwa
 upade wa washiriki wa mkutano huo kwa nyakati tofauti walisema kwamba 
mipango mbalimbali ya kimaendeleo inayopangwa na serikali inatakiwa 
kuwekewa vipaumbele kwa wananchi badala ya utekelezaji na tathimini 
kubakia ngazi za serikali kuu pekee.
Mkurugenzi
 Mtendaji wa Taasisi ya Utafiti wa Uchumi na Kijamii (ESRF), Dkt. Tausi 
Kida (kushoto) na Mkurugenzi wa Kupunguza Umaskini na Kuinua Uchumi 
kutoka Wizara ya Fedha na Mipango, Anna Mwasha wakinakili mambo muhimu 
wakati mgeni rasmi (hayupo piichani) akitoa nasaha zake.
Walisema
 kwamba katika utekelezaji wa Malengo ya Maendeleo Endelevu SDG’s ni 
lazima kutengeneza mpango mkakati wa mawasiliano wa masuala ya 
utamaduni, mila na desturi za jamii husika ambapo mipango hiyo inatakiwa
 kutekelezwa ili iwe rahisi wananchi kufahamu vizuri umuhimu wa mipango 
hiyo.
Washiriki
 hao walisema katika utekelezaji wa mipango hiyo ni lazima kuwepo na 
mikakati ya makusudi ya kuhakikisha changamoto ya umasikini uliokithiri 
unapungua kulingana na mikakati mbalimbali inayowekwa na vipaumbele vya 
kimataifa ili viweze kutekelezwa kwa vitendo na nchi husika.
Aidha
 wameshauri kwamba katika utekelezaji wa Malengo ya Maendeleo Endelevu 
SDG’s ni lazima kuzingatia suala la serikali za mitaa, kutumia lugha 
nyepesi katika mawasiliano, kufanya marejeo katika maandiko ya baadhi ya
 waasisi wa kitaifa akiwemo Mwalimu Nyerere na kufanya utafiti juu ya 
matumizi sahihi ya Rasilimali.
Pichani
 juu na chini ni wadau wa sekta za maendeleo visiwani Zanzibar 
walioshiriki katika mkutano wa kujadili utekelezaji wa Malengo ya 
Maendeleo Endelevu (SDG’s) visiwani humo ambao umefanyika katika Hoteli 
ya Zanzibar Ocean View.
Sambamba
 na hayo wamesema katika utekelezaji wa Malengo ya Maendeleo Endelevu 
(SDG’s) ni lazima kuweka kipaumbele kwa makundi maalum ya watu wenye 
mahitaji maalum wakiwemo Watu wenye Ulemavu.
Warsha
 hiyo imeandaliwa na Taasisi ya Utafiti wa Uchumi na Kijamii (ESRF) 
ambapo imewakutanisha wadau mbalimbali kujadili utekelezaji wa Malengo 
ya Maendeleo Endelevu (SDG’s) visiwani Zanzibar na kufadhiliwa na 
Shirika la Maendeleo la Umoja wa Mataifa (UNDP).
Mshauri
 wa Masuala ya Uchumi wa Shirika la Umoja wa Mataifa la Maendeleo (UNDP)
 Tanzania, Rogers Dhliwayo akiwasilisha mada katika mkutano wa wadau wa 
sekta za maendeleo nchini wa kujadili utekelezaji wa Malengo ya 
Maendeleo Endelevu (SDG’s) visiwani Zanzibar.
Kutoka
 kushoto ni Mwakilishi wa Umoja wa Mataifa (UN) Ofisi ya Zanzibar, Anna 
Senga, Mkurugenzi wa Idara ya Ushirikiano wa Kimataifa wa Wizara ya 
Mambo ya Nje, Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Kikanda na Kimataifa, 
Balozi Celestine Mushy, mgeni rasmi Katibu Mtendaji wa Tume ya Mipango 
Zanzibar, Juma Reli, Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Utafiti wa Uchumi
 na Kijamii (ESRF), Dkt. Tausi Kida (kushoto) pamoja na Mkurugenzi wa 
Kupunguza Umaskini na Kuinua Uchumi kutoka Wizara ya Fedha na Mipango, 
Anna Mwasha wakiwa meza kuu.
Naibu
 Katibu Mkuu Wizara ya Kazi, Uwezeshaji, Wazee, Vijana, Wanawake na 
Watoto ya visiwani Zanzibar, Mauwa Makame Rajab akitoa maoni katika 
mkutano wa wadau wa sekta za maendeleo nchini wa kujadili utekelezaji wa
 Malengo ya Maendeleo Endelevu (SDG’s) visiwani Zanzibar uliofanyika 
katika Hoteli ya Zanzibar Ocean View.
Mkurugenzi
 wa Idara ya Ushirikiano wa Kimataifa wa Wizara ya Mambo ya Nje, 
Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Kikanda na Kimataifa, Balozi Celestine 
Mushy (kushoto) na Katibu Mtendaji wa Tume ya Mipango Zanzibar, Juma 
Reli wakisikiliza maoni ya wadau yaliyokuwa yakiwasishwa kwenye mkutano 
kuelekea utekelezaji wa SDGs.
Bw.
 Sefu Mwinyi kutoka Tume ya Mipango Zanzibar akiwasilisha maoni yake 
katika mkutano huo uliowakutanisha wadau wa sekta za maendeleo visiwani 
Zanzibar.
Katibu
 Mkuu Wizara ya ya Elimu na Mafunzo ya Amali visiwani Zanzibar, Khadija 
Juma (kushoto) akichangia hoja katika mkutano huo. Kulia ni Katibu Mkuu 
Ofisi ya Rais, Katiba, Sheria, Utumishi wa Umma na Utawala Bora visiwani
 Zanzibar, Asha Abdallah Ali.
Mgeni rasmi katika picha ya pamoja na washiriki wa mkutano huo.
 
 
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni