ENGLAND 'MAKELELE' WANG'OLEWA EURO NA ICELAND
Pamoja
 na kutokuwa na mafanikio makubwa sana katika michuano ya kimataifa, 
England ndiyo wanaongoza kwa kuwa na makelele mengi na leo, wameng’olewa
 kwenye michuano ya Euro kwa kuchapwa mabao 2-1.
Mabao hayo 2-1 yametoka kwa Iceland ambayo awali ilionekana ni kibonde na isiyo na uwezo.
Lakini
 imefanikiwa kuonyesha soka safi, ikitoka nyuma na kusawazisha halafu 
ikafunga bao la pili. England walianza mapemaa kwa bao la penalti la 
nahodha Wayne Rooney.
Lakini
 mwisho, England wakatoka na kuacha gumzo kwani Iceland inakwenda nusu 
fainali ikiwa iliingia katika michuano hiyo haipewi hata nafasi ya 
kuvuka hatua ya makundi.
 

 
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni