Watumishi wa Umma waaswa kuzingatia maadili katika kutekeleza majukumu yao
—————————–
Watumishi wa Umma waaswa kuzingatia maadili katika kutekeleza majukumu yao hasa wanapowahudumia wananchi ili kuongeza tija.
Kauli
 hiyo imetolewa leo Bungeni Mjini Dodoma na Waziri Mkuu wa Jamhuri ya 
Muungano wa Tanzania Mhe. Kassim Majaliwa wakati wa kipindi cha maswali 
ya papo kwa papo kwa Waziri Mkuu.
Akifafanua
 Mhe. Majaliwa amesema kuwa ni dhamira ya Serikali kuhakikisha kuwa 
watumishi wote wa Umma wanazingatia uadilifu, uchapakazi, sheria, 
taratibu na kanuni zinazosimamia Utumishi wa Umma.
“Serikali itawachukulia hatua kali wale wote watakaotumia madaraka yao vibaya bila kujali vyeo vyao” alisisitiza Mhe. Majaiwa.
Katika
 hatua nyingine Mhe. Majaliwa amesema kuwa Serikali hivi karibuni 
itawasilisha Bungeni muswaada wa Sheria utakaosaidia kuanzishwa Kwa 
Divisheni ya kushughulikia Mafisadi katika Mahakama Kuu.
Lengo
 la Serikali ni Kuhakikisha kuwa wananchi wanahudumiwa vizuri pale 
wanapohitaji huduma mbalimbali ndio sababu tunaendelea kuimarisha vyombo
 vyetu kama Taasissi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU) ili 
zitekeleze majukumu yake vizuri.
Katika
 kuimarisha maadili Mhe. Majaliwa amesema kuwa Serikali inaangalia 
uwezekano wa kuanza kujumuisha masomo ya maadili katika mitaala ya Elimu
 hapa nchini ili kuongeza kasi ya kukuza na kujenga maadili miongoni mwa
 jamii.
 
 
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni