Watumishi wa Umma waaswa kuzingatia maadili katika kutekeleza majukumu yao
—————————–
Watumishi wa Umma waaswa kuzingatia maadili katika kutekeleza majukumu yao hasa wanapowahudumia wananchi ili kuongeza tija.
Kauli
hiyo imetolewa leo Bungeni Mjini Dodoma na Waziri Mkuu wa Jamhuri ya
Muungano wa Tanzania Mhe. Kassim Majaliwa wakati wa kipindi cha maswali
ya papo kwa papo kwa Waziri Mkuu.
Akifafanua
Mhe. Majaliwa amesema kuwa ni dhamira ya Serikali kuhakikisha kuwa
watumishi wote wa Umma wanazingatia uadilifu, uchapakazi, sheria,
taratibu na kanuni zinazosimamia Utumishi wa Umma.
“Serikali itawachukulia hatua kali wale wote watakaotumia madaraka yao vibaya bila kujali vyeo vyao” alisisitiza Mhe. Majaiwa.
Katika
hatua nyingine Mhe. Majaliwa amesema kuwa Serikali hivi karibuni
itawasilisha Bungeni muswaada wa Sheria utakaosaidia kuanzishwa Kwa
Divisheni ya kushughulikia Mafisadi katika Mahakama Kuu.
Lengo
la Serikali ni Kuhakikisha kuwa wananchi wanahudumiwa vizuri pale
wanapohitaji huduma mbalimbali ndio sababu tunaendelea kuimarisha vyombo
vyetu kama Taasissi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU) ili
zitekeleze majukumu yake vizuri.
Katika
kuimarisha maadili Mhe. Majaliwa amesema kuwa Serikali inaangalia
uwezekano wa kuanza kujumuisha masomo ya maadili katika mitaala ya Elimu
hapa nchini ili kuongeza kasi ya kukuza na kujenga maadili miongoni mwa
jamii.
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni