Shilingi 137 Milioni zahitajika kufunga vifaa hospital ya Benjamin Mkapa Dodoma
Waziri
 wa Afya,Maendeleo ya Jamii,Jinsia,Wazee na Watoto,Ummy Mwalimu 
(katikati) akikagua majengo ya hospitali ya Benjamin Mkapa iliyopo Mjini
 Dodoma,kulia ni Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa hospitali Hiyo Profesa Ainory 
Gessase.
Kaimu
 Mkurugenzi Mkuu Profesa Ainory Gessase(mwenye koti jeupe)akimfafanulia 
jambo waziri wa Afya wakati alipotembelea hospitalini hapo na kujionea 
jinsi wanavyotoa huduma kwa wananchi
Waziri
 Ummy Mwalimu akikagua baadhi ya vifaa tiba vilivyopo kwenye hospitali 
hiyo ambapo zinahitajika shilingi milioni 137 za kitanzania kuweza 
kufunga vifaa vya kiuchunguzi vya magonjwa ya moyo na figo.
…………………………………………………………………………………………..
Na.Catherine Sungura ,Dodoma
 Serikali kupitia Wizara ya Afya 
inatarajia kuzindua huduma zote Za kiuchunguzi za magonjwa kwenye 
hospitali ya kisasa ya Benjamin Mkapa iliyopo mjini Dodoma
 Hayo yamesemwa leo na waziri wa 
Afya,Maendeleo ya Jamii,Jinsia,Wazee na Watoto Ummy Mwalimu wakati 
alipotembelea hospitali hiyo na kuona inavyoendelea kutoa huduma za afya
 kwa wananchi
 Waziri Ummy alisema serikali 
imejipanga katika kutekeleza ahadi yake kwa wananchi katika utoaji 
huduma bora na za kisasa katika hospitali hiyo
 “Nawaahidi nitafanya uzinduzi 
rasmi wa huduma za uchunguzi wa magonjwa ili wananchi waelewe hospitali 
yetu inatoa huduma zipi ili kila mwananchi atambue nini kinapatikana 
hapa”alisema Mhe.Ummy
  Aidha,Waziri Ummy alisema licha
 ya kazi nzuri inayofanywa na watoa huduma wa afya wa hospitali hiyo 
bado inakabiliwa na changamoto kubwa ikiwemo kukatika kwa umeme mara kwa
 mara na kuahidi kuwasiliana na wizara ya Nishati na Madini ili kutatua 
tatizo hilo.
 Haha hivyo alisema wizara yake 
inafuatilia upatikanaji wa fedha kiasi cha shilingi milioni 137 za 
kukamilisha ujenzi wa ufungaji wa baadhi ya vifaa tiba vilivyopo 
hospitalini hapo na hivyo kuwakaribisha wananchi wote kufika hospitali 
hapo kupata huduma za kibingwa za ugonjwa wa kisukari
 Mhe Ummy amesisitiza kuanza 
kutolewa kwa huduma za vipimo (kama MRI na CT Scan) katika Hospitali 
hiyo ili kuwapunguzia kero wananchi wa mikoa ya kanda ya kati kupata 
huduma hizo Dodoma badala ya kusafiri hadi Dar es salaam kupata huduma 
hizo.
 Hospitali ya Benjamin Mkapa ipo 
katika chuo kikuu cha Dodoma,kwa sasa inahudumia wagonjwa zaidi ya 170 
kwa siku,ikikamilika itakua inafanya uchunguzi wa magonjwa ya 
figo,kisukari pamoja na moyo
 
 
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni