Sekta binafsi ishirikishwe katika utekelezaji wa Mpango
Kaimu
 Katibu Mtendaji wa Tume ya Mipango, Bibi Florence Mwanri akizungumza 
wakati wa kufunga mkutano wa Wachumi na Maafisa Mipango uliofanyika 
katika ukumbi wa Hazina, Dodoma.
………………………………………………………………………………………………
Na Joyce Mkinga
SEKTA Binafsi katika ngazi zote ni
 lazima ishirikishwa katika utekelezaji wa Mpango wa Taifa wa Maendeleo 
2016/17 – 2020/21 uliozinduliwa hivi karibuni.
Kaimu Katibu Mtendaji wa Tume ya 
Mipango Bibi Florence Mwanri aliyasema hayo alipokuwa akifunga mkutano 
wa Wachumi na Maafisa Mipango uliofanyika mjini Dodoma mwishoni mwa 
wiki.
Bibi Florence Mwanri amesema sekta
 binafsi ni wadau muhimu katika utekelezaji wa Mpango wa Taifa wa 
Maendeleo hivyo, wanatakiwa kushirikishwa katika mipango yote ya 
Serikali.
“Katika mipango yetu katika ngazi 
zote lazima sekta binafsi ishirikishwe kwa sababu wao ndio watekelezaji 
wakubwa wa mpango huo” alisema Bibi Mwanri
Amesema maafisa mipango wanapoibu 
miradi mbalimbali katika ngazi ya kijiji, wilaya, mkoa ni lazima sekta 
binafsi ishirikishwe ili kuwapa fursa nzuri ya kushiriki kikamilifu 
katika utekelezaji wa Mpango wa Taifa wa Maendeleo ambao unalenga katika
 Kujenga Uchumi wa Viwanda ili Kuchochea Mageuzi ya Kiuchumi na 
Maendeleo ya watu
Mkutano huo uliwashirikisha 
wachumi na maafisa mipango 170 kutoka katika wizara, idara za serikali, 
sekretarieti na mikoa na wilaya, taasisi za utafiti, na sekta binafsi 
ulikuwa na kaulimbiu ya Kuelekea kwenye Utekelezaji wa Mpango wa Taifa wa Maendeleo 2016/17 – 2020/21.
Lengo kuu la Mkutano huo ilikuwa 
ni kujenga uelewa wa pamoja juu ya Mpango wa Taifa wa Maendeleo wa Miaka
 Mitano na utelekezaji wake.
Mpango huo unatarajia kugharimu Trilioni 107 ambapo Sekta binafsi itachangia  Trilioni 48.
Akiwasilisha maazimio ya mkutano 
huo Kaimu Naibu Katibu Mtendaji wa Tume ya Mipango kutoka Klasta ya 
Uchumi Jumla, Dkt. Lorah Madete amesema Serikali na sekta binafsi 
wakutane pamoja na kupanga mikakati ya kutekeleza mpango huo wa 
maendeleo.
Vile vile, Dkt Madete alisema kuwa
 kuna haja ya Serikali kuingiza Malengo ya Maendeleo Endelevu ya Dunia 
katika mipango ya Serikali ikiwa ni pamoja na Mpango wa Taifa wa 
Maendeleo wa Miaka Mitano.
Mkutano huo uliandaliawa Tume ya Mipango kwa ushirikiano na Taasisi ya Uongozi
 
 
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni