Ulinzi vituo vya DART kuimarishwa
Baadhi ya abiria wanaotumia 
usafiri wa mabasi yaendayo kasi maarufu kama mwendo kasi wameilalamikia 
kampuni hiyo kwa kushindwa kudhibiti vitendo vya wizi vinavyoendelea 
katika baadhi ya vituo hivyo.
Bw. Juma Ally mkazi wa Kimara 
mwisho anasema vitendo hivyo hutokea nyakati za usiku kwa baadhi ya 
vijana kujifanya nao ni miongoni mwa watumiaji daraja hilo na kupelekea 
abiria kuibiwa vitu vyao ikiwa ni pamoja na kujeruhiwa.
Aliongezea kuwa walinzi wa kituo 
hicho wamekuwa wakifanya kazi ya kuwapanga abiria na kusahau majukumu 
yao ya kulinda usalama wa kituo hicho pamoja na mali zao.
“Tunashangaa hawa walinzi 
wanaolinda vituo hivi, abiria wamekuwa wakilalamika kila siku kuibiwa 
nyakati za usiku lakini tunaona abiria wakiendelea kuibiwa sijui 
wahusika wapo wapi?”Aliuliza Bw. Ally.
Nae Bi. Herrieth Shangaa 
aliongezea kuwa licha ya vitendo vya wizi vinavyoendelea katika vituo 
hivyo kuna baadhi ya vitendo vikiwemo vya kujisaidia katika madaraja 
hayo hivyo kupelekea uchafuzi wa mazingira
Akizungumza na mwandishi wa habari
 hizi msimamizi wa vituo hivyo ambae hakutaja kutajwa jina lake amesema 
kuna baadhi ya vituo ni vikubwa na wanawalinzi wachache hivyo 
wamejipanga kuongeza ulinzi ikiwa ni pamoja na kufunga mfumo wa 
kidigitali wa kudhibiti wahalifu
Mradi wa mabasi yaendayo haraka 
ulioanza rasmi terehe 10, mei, 2016 umeonesha ni jinsi gani kero ya 
foleni itakavyopungua kwa kuwa mabasi hayo yanatumia njia yake ambayo ni
 miundombinu  iliyojengwa kwa  gharama kubwa  sana.
 
 
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni