ZLATAN, MAN UNITED WAMALIZANA, ATATANGAZWA RASMI IJUMAA
Baada
 ya kusubiriwa kwa muda mwingi, hatimaye Manchester United inatarajia 
kumtangaza rasmi Zlatan Ibrahimovic kuwa mchezaji wake mpya.
Zlatan,34, atatangazwa Ijumaa hii kuwa mchezaji wa Man United iliyo chini ya Jose Mourinho.
Raia
 huyo wa Sweden amemaliza mkataba wake na PSG ya Ufaransa ambako 
alifanya vema baada ya maisha yake ya soka akiwa Ajax nchini Uholanzi 
baadaye nchini Italia akiwa na Juventus, Inter Milan na AC Milan, pia 
Barcelona ya Hispania.
 

 
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni