Makamu wa Rais awataka wakuu wa wilaya na mikoa kukamilisha zoezi la madawati kabla ya June 30.
Na Daudi Manongi,MAELEZO
Makamu wa Rais Mhe Samia Suluhu 
amewataka wakuu wa wilaya na mikoa kuhakikisha wanamaliza zoezi la 
upatikanaji wa madawati kwa shule za msingi na sekondari.
Mhe. Suluhu ameyasema hayo leo 
Ikulu Jijini Dar es Salaam wakati wakuu wa wilaya na mikoa walipokuwa 
Ikulu wakila kiapo cha maadili ya viongozi kabla ya kwenda kuapishwa na 
wakuu wa mikoa yao.
Aidha amewaagiza viongozi hao 
kusoma alama za nyakati kwa kuangalia makosa ya waliokuwepo kabla yao 
ili kuhakikisha hawarudii makosa yaleyale.
Mhe.Suluhu pia amesema kuwa 
Serikali haitaki kusikia wananchi wanalia njaa na hivyo wakuu wa wilaya 
wahakikishe chakula kinapatikana katika maeneo yao kwani hilo ni jukumu 
lao.
Aliongeza kuwa wakuu wa wilaya 
wana majukumu makubwa ya kuhakikisha wananchi wanapata huduma zote za 
muhimu katika maeneo yao kwani wananchi wana mategemeo makubwa juu yao.
Aidha ameagiza wakuu wa Wilaya 
hao kufanya kazi karibu na Maafisa Tarafa ili kujua kero za wananchi na 
kuzifanyia kazi kwa kasi ili wananchi wafaidike na maendeleo yawafikie 
kwa haraka.
Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais, 
Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (Tamisemi), George Simbachawene 
 ivi karibuni aliwaagiza wakua wa wilaya na mikoa kuhakikisha wanatimiza
 agizo la Rais John Pombe Magufuli kuhakikisha hakuna mwanafunzi 
atakayekaa chini kwa uhaba wa madawati kufikia June 30,2016.
 
 
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni